Ilikuwa majira ya asubuhi, Rama akiwa anaendesha gari kuelekea kazini. Ni muda ambo alikuwa anawahi kazini kwenye kikao na wakurugenzi. Rama alikuwa anaendesha gari alilopewa na ofisi ili kuongeza ufanisi kwake ikiwemo kuwahi kazini.
Siku hii kulinyesha mvua kiasi. Baadhi ha njia zikawa na foleni. Sasa wakati Rama aneendesha alifika sehemu iliyomshangaza kidogo....
Ukiachana na Main Road kulikuwa na njia ya chocho, ambayo magari mengi yalikuwa yanapita. Huku nyingine hakuna gari lolote lililokuwa linapita. Akajiuliza sababu na kuikosa. Na jana yake wakati anatoka kazini ndiko alikopitia. Rama akaanza kujiuliza juu ya nini afanye. Awafuate wengine au ajitose kwenye njia ya peke yake.
Wakati anawaza zikaja gari nne nyuma yake na zote zikapita kwenye njia nyingine ya chocho. Kwa kuwa aliona magari yote yanapita katika njia hiyo. Bila kuuliza na yeye akaamua kuungana nao. Dakika chache baadaye simu ikaita bosi wake anauliza kama amefika.
Rama: Helow! Boss!huki akiwa ameshika kichwa afanye nini, kule alikoingia gari nyingi hawezi kutoka tena. Njia ni ndogo. Kwa sababu kila mtu alikuwa anapita katika njia hiyo.
Bosi: Uko wapi kijana wangu?
Rama: Mhh! Yaani! Unajua Bobosii! Nipo hapa sio mbali na barabara kuu. Kuna chocho tumeingia kuna msongamano wa magari.
Boai: Msongamano wa magari? Mhh mbona dakika chacha nimetoka huko hamna foleni.
Rama:Sasa kilichotokea, nilifika kwenye kinjia pale kati nikaona watu wote wanapita nikaacha Main Road nikaunga. Japo niliwaza kitu kama hicho kukazania main road. Ila baadaye nikaona magari mengi yanapita njia hii nikaliunga. Kwa hiyo tunafanyaje bosi? Bosi: Nadhani huu mradi tushaukosa ila wewe ndio responsible.
Ndio maana tulikupa gari ili uwahi. Ni nini umefanya? Muda wa kikao umefika.
Rama: Mhhh hapana bosi..je, naweza kukuuliza? Boss ndio kijana wangu.
Rama: Ingekuwa ni wewe, unaona watu wote wanapita njia ya chocho. Huku Main Road hakuna anayeendelea kwenda mbele ungepita njia hii?
Bosi:Mhh ngoja kwanza nimeitwa ntakucheki baadaye.
Rama: Helow Boss Helow boss.
Sime imekatwa. Hakuweza kutoa jibu.
Sasa kwako mpendwa msomaji. Ingekuwa ni wewe ungepita njia hii?
Nini tunajifunza?
Kwanza hapo juu bosi alikata simu. Kwanini alikata simu? Swali aliloulizwa na Rama lilimpa utata sana. Aliona mazingira yalivyo. Ili kuyaepuka akakata simu.
Ila Rama hakuuliza kujua kwa nini njia kuu haipitwi na hakuna kibao kinachoonyesha njia imezuiwa. Hivi ndivyo tunavyokutana na vishawishi maishani mwetu.
Kumbe, kwenye maisha kila mtu anazo njia zake. Anayo safari yake. Anayo matarajio yake. Ikiwa huna yako, jua utaenda kukamilisha ya wengine.
Chocho lako lipo katika kazi zako, familia yako, biashara yako. Lakini ili uyashinde yote haya. Baki njia kuu. Wengi wanapenda sana njia za mkato. Na unapofika kule kujitoa sio kazi ndogo.
Wakati ndio huu kubaki katika njia kuu ambayo wengi wanaikataa. Ni njia iliyowazi kumfanye yeyote aliyejipanga kufikia hatma ya safari yake. Karibu tupite wote njia kuu.
Mungu akubariki sana. Karibu tujifunze zaidi.
Bonga nasi hapa hapa
Imeandaliwa na Lackius Robert. 0767702659
Mwangaza2023
No comments:
Post a Comment