Saturday, August 17, 2019

Vijue vichocheo vya mgogoro ili uishinde migogoro

MORNING MOTIVATION DIARY

Vichocheo vya migogoro:

Ndugu,
Ni siku nyingine tena tunakutana katika morning motivation diary yenye lengo kubwa kuongezea maarifa na kuing'alisha siku yako.
Karibu katika mwendelezo wa vichocheo vya migogoro:

Ubaguzi (Descrimination) Kuna baadhi ya watu wamekuwa wakibaguliwa miongoni mwa sehemu za kazi kutokana hali fulani fulani.
Ukiangalia sheria ya ajira na mahusiano kazini ya mwaka 2004 kifungu kidogo cha 7 inakataza ubaguzi wa aina yoyote katika sehemu za kazi iwe rangi,ugonjwa ,dini,kabila,.
Hivyo katika sehemu ya kazi ikitokea mtu kubaguliwa mgogoro mkubwa unaibuka kwa sababu ,inaonesha thamani yake aionekani ,pia mchango wake hauonekani kuthaminiwa.Binadamu sote ni sawa tukiondoa tofauti zetu za kikabila kidini.

Matarajio usiyoyatarajia (unrealistic expectations).
,Hali huchochea  migogoro zaidi hasa pale ambapo mmojawapo anapokuwa anatarajia kupata kitu Fulani.Mfano Mshahara labda mwisho wa mwezi ikatokea hajaupata hivyo siku zimeongezwa mbele. Labda ameongeza elimu akitarajia kupandishwa cheo(promotion) na kuongezeka kwa bonus lakini hivyo vyote vikawa havijatendeka.Matarajio yake yanakuwa tofauti na alivyoyanga hivyo usababisha kuongezeka kwa mgogoro kati yake na wshusika ofisini.Inaweza kusababisha presenteism yani mfanyakazi yupo kama hayupo kazini.

Mawasiliano hafifu,
Ili kazi iweze kufanikiwa zaidi inahitaji uwepo wa ushikiriano mzuri unaoambatana na mawasiliano mazuri.
Maana kila mmoja atatimiza wajibu wake ikiwemo kuhudhulia mikutano husika ikihitajika,kubadilisha mawazo na mambo mengine ili kazi ziweze kwenda zaidi.
Mawasiliano yanategemea sana maneno inabidi kuhakikishia kuwa mawasiliano yako yanaenda zaidi ya maneno.Ikiwa unazungumza na mtu mmoja au zaidi tambua maneno pia matendo yanaweza kuathiri uhusiano wako pamoja na ukweli utakaoutoa kutumia maneno sahihi na hisia sahihi, wakati wa kuzungumza na mtu.

Pindi mawasiliano yakosapo kuna baadhi ya kazi hazifanyiki kwa wakati kitu kinachopelekea mgogoro kuibuka.

Kukosekana uaminifu ,Kuna usemi unaosema uaminifu ni mtaji.Hivyo katika sehemu za kazi ata ili ufanisi uongezeke uaminifu inabidi uwepo.Kwa maana ya kwamba mfanyakazi anaweza achiwa kazi zingine kama anaaminiwa akazimalizia bila ofu.

Lakini kama uaminifu aupo miongoni mwa wafanyakazi hali hii husababisha baadhi kukosa fursa,au kutopewa kazi badala yake wanapewa waaminifu.Hali hii huibua mgongano mkubwa kwanini wengine wanaachiwa au kupewa kazi ama pengine kupandishwa vyeo na wengine hawapandishwi. Je hali ikoje katika sehemu unayofanyia kazi?. Wish you all the best let's meet on the next discussion.

"Ushindi upo mikononi mwako kwa kuwa umebarikiwa".

Kwa mawasiliano zaidi 0767702659 Lackius Robert

No comments:

Post a Comment