Tuesday, November 10, 2020

UKIANGUKA MARA 7 INUKA YA 8,Hadithi ya muigizaji wa movie ya TITANIC 1998.

Ndugu Karibu katika mwendelezo wa masomo yetu yanayolenga kukuongea maarifa zaidi,leo tunaenda kuangalia hadithi ya muigizaji wa movie ya TITANIC.

Ukianguka Mara 7 mara ya 8 amka uendelee na safari.Huo ni msemo uliojitokeza kwa muigizaji maarufu duniani Leonard Di Caprio ambaye aliigiza movies maarufu kama vile  Titanic,Aviator,Blood Diamond. Kwa mara ya kwanza aliandika historia kama best male actor,  kabla ya hapo aliwahi kuchaguliwa kuingia kwenye kinyanganyilo cha best male actor  zaidi ya mara tano tangu 1994 lakini alikuja kufanikiwa kupata tuzo hiyo mwaka 2016 baada ya miaka 22 kupita.

Wakati wote alikuwa anasubira ya kuwa siku moja atakuja kuipata tuzo hiyo na ilipofika watazamaji walidhani kitu cha  kwaida lakini haikuwa hivyo kwake ilikuwa ni heshima kubwa.Alichoka kushiriki na wenzake katika kinyanganyilo hicho.Lakini siku ilifika akaweza kupata tuzo hiyo aliyoifukuzuia kwa miaka zaidi ya 22.

Nikukumbushe ndugu yangu mpendwa kama bahati imeandikwa utaipata tu haiwezi kupotea kitu cha muhimu na msingi ni kuipalilia njia ili bahati ikutane na maandalizi.Haijalishi muda gani utapita ila utaipata tu,Jifunze uelimike zaidi ili uchukue hatua dhidi maisha yako kukata tamaa ni mwiko songa mbele amini katika ushindi.Pia tuache hali ya kualalamika maana kualalamika hakuwezi kuwa masaada kwetu ata siku moja.

Tafakari ndugu yangu mapendwa na uweze kuchukua ahtua juu ya amisha yako.
Makala hii imeandaliwa na Lackius Robert tuwasiliane zaidi 0767702659 karibu mungu akubariki zaidi.

Monday, November 09, 2020

UMOJA NI NGUVU,Hadithi ya muuza maziwa.

Habari za asubuhi ndugu yangu mpendwa karibu katika makala zetu kila siku ambapo unakuwa unapata neno linalokupa hamasa zaidi,leo tunaenda kuangalia hadithi ya muuza maziwa. 

Bwana mmoja alipata nafasi ya kuwa anapeleka maziwa katika hoteli fulani hapa mjini.Bwana huyo alikuwa akiwaza sana lini atapata sehemu angalau ya kupeleka bidhaa yake kwa muda mrefu. Alipofanikiwa kuipata hotel ile alifurahi sana akaanza kuimba uku akishangilia kwa nyimbo na vifijo na ndelemo.Akajua utajiri upo njiani! muda sio mrefu nanunua garina mipango mingine mingi.

Aliweza kuelewana na wahusika na akaanza kutoa huduma hiyo ,ila jambo la  ajabu na la kushangaza ni kuwa ni aliweza kutoa huduma hiyo miezi miwili tu akawa ameishiwa hakuwa na maziwa tena.Alisahau kuwa "ujasiri hauwezi kukupa mafanikio ila unakupa nguvu ya kupambana na maisha".pia umoja ni nguvu utengano ni udhaifu alihitaji kufanya kazi hiyo peke yake na furaha ikageuka kuwa majuto.

Maziwa alikuwa anatoa kwa Ng'ombe zake mwenyewe zilipoacha kutoa ,tenda ikamshinda .Akapewa mtu mwingine mwenye uwezo na network nzuri ya wauza maziwa mengine kutika sehemu tofauti tofauti waliokuwa wanamletea maziwa.Akawa ana nguvu na support ya kutosha kupeleka maziwa hotelini tofauti na yule wa mwanzo.

Kuna wakati sisi tunalalamika kuwa hatupati fursa ,sisi ni watu wa bahati mbaya lakini ukweli ni kuwa tunazipoteza wenyewe.Mtu huyo alipoteza tenda hivi hivi sababu hakutaka kutengeneza network ya watu watakaomletea maziwa kwa bei nzuri tu ili aboreshe mahusiano na biashara yake.Tuitumie vizuri fursa tunayoipata.

Tunahitaji watu ili kuweza kusonga mbele zaidi ,natumaini lipo jambo umejifunza leo.Mimi ni Lackius Robert karibu tuendelee kujifunza zaidi tuwasiliane 0767702659 mungu akubariki.

Sunday, November 08, 2020

JINSI YA KUBRAND MAISHA YAKO 3.

karibu katika makala ya tatu na ya mwisho kutoka katika moja ya mafundisho ambayo aliwahi kutoa Jim Rhon enzi za uhai wake lipo jambo unaweza kujifunza, 

HATUA YA TATU 3. Usijaribu kwenda nje ya mfumo au kukimbizana na muda (DON’T TRY TO BEAT THE SYSTEM).

Ukweli ni kuwa mafanikio yanapitia mchakato mrefu kuona umeyafanikisha,watu wengi hukata tamaa pale wanapoona mambo hayaendi wamekutana na changamoto mbali mbali wanachoshindwa kujua ni kuwa kila kitu kina mfumo wake kinaenda kadili kilivopangwa.Wewe hupaswi kukimbizana na muda kama unaona umepata wazo na ukaanza kulifanyia kazi usikimbilie matokeo ya haraka tulia nenda taratibu hata kama itakuchukua muda upi kama uko katika njia sahihi matokeo utayona bila shida yoyote.

Unaweza kuwa uanjifunzaharaka lakini haimanishi kuwa ndo utegemee kupata matokeo haraka unahitaji muda na utulivu katika kuyapata matokeo.Niliwahi kuanguka mara 7 katika sehemu moja japo kwa vipindi tofauti watu wakawa wanasema kuwa si uache kile unachofanya maana hatuoni hatua unayopiga.Wengine hawawezi kuona hatua au maendeleo yako haaraka wewe ndiye unayekuwa unaona kwa sababu upo katika mfumo,unahitaji kuwa mtu wa kubadilika na kuenda na hali unayokutana nayo.

Kubali kupoteza pesa,nyumba gari na vinginevyo ila siyo AKILI YAKO maana akili yako ndipo kuna mipango yako yote unayotaka kufanya.Akili yako inaweza kukusaidia katika kutafuta mali zote zilizopotea,chunga sana itunze sana na iboreshe akili yako kila siku kwa kuilisha vitu endelevu na vyenye maana.

Tumia hatua hizi tatu kuyaboresha miasha yako kupitia kazi unazozifanya.

Makala hii imeandaliwa na Lackius Robert 0767702659 karibu tujifunze zaidi.

Pia nakukaribisha upate uchambuzi wa vitabu kwa njia ya kiswahili ili uweze kujifunza zaidi na kuongeza maarifa tuwasiliane zaidi.

JINSI YA KUBRAND MAISHA YAKO 2.

 HATUA YA PILI 2. GO TO WORK (NENDA KAFANYE ).

Ukiangalia katika hatua ya kwanza tumeona kuwa unahitaji kujua namna vitu vinavyopaswa kufanyika kwa kutumia mawazo yako.Baada ya hapo hatua inayofuata ni kuwa unapaswa kuchukua hatua kwa kile ulichoanzisha,hatua hizi ndizo zinazokuwa zinakupa nguvu na kukuonesha kuwa wewe ni mtu mwenye uthubutu mkubwa katika utendaji wako wa kazi.

Watu wengine wanapokuwa wanakufundisha labda siku za mwisho wa wiki au siku zingine hakikisha unachukua pointi za msingi sana unaweza kuwa unafundishwa katika uchumi au uwekezaji kamwe “usiruhusu kufanya kazi peke yako” unahitaji pia kupata mawazo ya watu wengine ili kuweza kuyaunganisha na mawazo yako.

Kuna mtu alitaka kuniambia kitu nikamwambiaje kabla ujaniambia nioneshe (don’t tell me, show me) usiniambie nioneshe akimaanisha matendo yanaongea kuliko maneno.Fanya zaidi juu ya kitu unachotaka kufanya.Kadili unavyokuwa unachukua hatua mara kwa mara ndivyo unavyokuwa unapata uzoefu na kuondoa hofu ya kuanza anasema massive action ‘the cure all’kuchukua hatua kunanitbu yote.

Tumia kanuni hii katika kila wazo zuri chukua hatua take good idea –take action , Hakikisha unakuwa na mawazo mengi uwezavyo ili uweze kuwa na nafasi ya kuchambua ya msingi.Usipofanyia kazi kile unachojifunza utakuwa mjinga unakpaswa kujitahidi kuwa mtu wa kuchukua hatua mara zote upatapo wazo zuri.

Tumia maarifa unayojifunza kama njia ya kukupeleka katika utajiri.Utajiri ninaouzungumzia siyo utajiri wa pesa maana pesa ni sehemu tu inayotokana na zao la thamani.Nawajua watu wengi wenye pesa lakini ni maskini.Pesa hazikupangii kitu cha kufanya wewe ndiye unayepaswa kuzipangia kama una mipango mingi pesa yako itazidi kukuua na kuzaa zaidi ila kama huna mipango pesa yako haitaweza kuzaa badala yake itapotea bila kujua.

Usikose sehemu inafuata na ya mwisho.

Mimi ni Lackus Robert 0767702659 karibu sana na mungu kaubariki zaidi.

JINSI YA KUBRAND MAISHA YAKO 1.

Habari za asubuhi ndugu yangu mpendwa karibu katika mwendelezo wa makala zetu kila siku ,leo tunaenda kuangalia namna unavyoweza kubrand maisha yako na kuwa mapya hizi zilitolewa na Jim Rohn katika mfululuzo wa mafundisho yake. 

HATUA YA KWANZA 1.FIND HOW THINGS WORK(TAFUTA KUJUA NAMA VITU VINAVYOFANYIKA).

Katika mchakato wa kujua namna gani vitu hufanyika unahitaji kuwa na( IDEA )wazo.Mawazo ya jinsi gani unaweza kutengeneza pesa,namna gani unaweza kufanya kazi zako kwa ubora na vitu vingine vya msingi.Katika hilo ni kwamba mawazo yoyote unayoyapata kuhusu kitu chochote kizuri unahitaji kuyaandika mahali au katika kijitabu chako kidogo ili ukiyahitaji iwe ni rahisi kuyapata anasema “Usitumie kichwa chako kutafuta mafaili yaliyojaa mawazo yako” anachomaanisha ni kuwa unaweza kusahau muda wowote hivyo weka mawazo yako katika maandishi,Ukiyahitaji utayapata haraka na bila kuangaika kwa kukuna kichwa chako uku ukifikiria mawazo uliyoyawaza.

Kwa kutumia mawazo tafuta namna mambo yanavyofanya kazi,

*      Kama unahitaji kufanikiwa soma mafanikio ya wengine kupitia usomaji huo unakuwa unapata mawazo mapya na mengi ambayo yanakusaidia kukuza uelewa wako.

*      Kama unataka kufurahia soma mawazo yanayofurahisha.

*      Kama unataka kuwa na afya njema soma makala zinazofundisha afya njema.

Usimalize siku bila kusoma chochote, unapaswa kusoma vitu vitakavyoweza kubalisha uchumi wako,jamii yako,imani yako na maisha yako kiujumla.Inawezekana usifanikishe kupata kila kitu unachokitaka ila ukapata vichache ,kupitia hivyo vichache hakikisha unatafuta na kujua namna kitu kinachofanyika.

Wengi wetu tunapata changamoto ya ukosefu wa habari za muhimu ,hakikisha unapata habari za muhimu na nzuri zitakazo kusaidia kujenga uelewa wako kila siku.

 Kuwa kama mtoto pale unapotaka kujua kitu.

Kuwa na furaha kama watoto hata wakati mgumu,mfano angalia watoto walivyo unaweza kumpiga baada ya dakika chache anakuwa amesahau kuwa umempiga anaruhusu maisha mengine yaweze kuendelea.

Usikose kufatria hatua ya pili katika makala inayofuata.

mimi ni Lackius Robert karibu sana tuendelee kujifunza zaidi 0767702659 au maarifarobert.com.

Mungu akubariki zaidi.

IPO NJIA MOJA YA KUPATA,Usikazanie zingine:

Habari za saa hizi ndugu yangu mpendwa karibu katika mwendelezo wa makala zetu kila siku zenye lengo la kukuongezea maarifa kila siku.Siku ya leo nimekuandalia vitu kadhaa kutoka kwenye kitabu cha 101 Crucial Lesson they dont teach you in your Business School Ways  chake Chris Haroun naamini lipo jambo utaweza kujifunza na kuchukua hatua.

Karibu sana,

=•Ipo njia moja ya kupata chochote unachotaka na njia hiyo ni kuomba. Ombeni na mtapewa ni siri muhimu ya mafanikio kwenye biashara. Kama kuna kitu unataka, omba na wengine watakuwa tayari kukupa, Huwezi kupata kitu bila kuomba bila kuomba utapata lakini utachelewa.

=•Biashara ni watu, haijalishi unajua nini, bali unamjua nani na nani anakujua wewe. Hivyo kazana kukuza zaidi mtandao wako wa watu unaowajua na wanaokujua.

=•Mchukulie kila mtu unayekutana naye kama mtu mashuhuri, jua ni mtu muhimu, muoneshe umuhimu na watu watapenda kukutana na wewe.Ili kufanikiwa kwenye biashara unahitaji kutengeneza marafiki wengi.

=•Tenga muda wa kufanya kazi sana na kisha tenga muda wa mapumziko. Tenga juma moja la kupumzika kila baada ya miezi sita.  Na unapotoka kwenye mapumziko, tenga tarehe ya mapumziko yanayofuata. Kadiri unavyofanya kazi sana ndivyo mwili wako unahitaji mapumziko pia, la sivyo utapata uchovu mkubwa utakaokukwamisha.

=•Msongo utakuua. Epuka sana msongo kwenye maisha yako. Msongo unatokana na hofu ambazo mtu anakuwa amejijengea, ondokana na hofu ulizonazo na hutakuwa na msongo. Jua kila kitu kitakwenda vizuri kama utachukua hatua sahihi.

=•Unapogundua una msongo mkali, jipe siku ya mapumziko, hata kama huumwi. Mapumziko haya yatapunguza msongo kwa kujiweka mbali na kazi. Lakini pia yatakuepusha kufanya makosa pale unapofanya maamuzi ukiwa na msongo.

=•Glasi imejaa mara zote. Ipo njia ya kupima mtazamo wa mtu, kwa kuweka maji nusu glasi kisha kumuuliza mtu aeleze glasi na maji. Wenye mtazamo chanya wanasema glasi imejaa nusu, wenye mtazamo hasi wanasema glasi iko tupu  nusu. Wenye mtazamo wa kujiamini wanaona glasi imejaa mara zote. Mara zote chukulia kile unachokutana kwa mtazamo chanya na jiulize unawezaje kunufaika nacho zaidi.

=•Sehemu kubwa ya hofu ulizonazo unajidanganya mwenyewe. Akili zetu zipo vizuri sana kwenye kutengeneza hofu, huwa zinatabiri mambo yatakuwa mabaya zaidi. Lakini mara zote mambo huwa hayawi mabaya kama tunavyotegemea. Hivyo usisikilize sana hofu zako.

=•Furahia kushindwa kwako. Hakuna mtu aliyewahi kufanikiwa sana bila ya kushindwa. Hivyo unaposhindwa furahia, kwa sababu ni njia ya kuelekea kwenye mafanikio makubwa.

=•Fedha siyo sawa na furaha. Lengo lako kuu kwenye kile unachofanya lisiwe fedha, bali anza kwa kupenda kile unachofanya na kutoa mchango wako kwa wengine. Na furaha unayoweza kuipata kwenye fedha ni kuwasaidia wengine.

Asante sana naamini lipo jambo umejifunza kazi kwako kuchukua hatua ,pia nakukaribisha upate chambuzi mbali mbali za vitabu kwa lugh ya kiswahili jiunge nasi ili uweze kujifunza kila siku na uboreshe kazi zako kupitia usomaji wa vitabu,utatumiwa kwenye WhatApp ,email pamoja na Telegram Mungu akubariki tuwasiliane 0767702659 Lackius Robert.


Thursday, November 05, 2020

HUWEZI KUFANANA NA SISI,Hadithi ya Mbwa Mwitu na Digidigi.

Habari za asubuhi ndugu yangu mpendwa karibu katika mwendelezo wa makala za kila siku kupitia blog hii,lengo kuu ni kukuongezea maarifa zaidi.

Leo tunaenda kupata funzo kutoka kwenye hadithi ya Digidigi pamoja na Mbwa Mwitu lipo jambo utajifunza karibu,

Siku moja Mbwa mwitu alikuwa katika harakati za mawindo msituni,Mara gafla akakutana na kundi moja la Digidigi wametulia wanakula majani kwa sababu alikuwa ana njaa kali ikabidi aanze kunyatia nyatia ili aweze kumshika mmoja wapo ajipatie kitoweo.Lakini kadri muda ulivyokuwa unazidi kwenda ndivyo wanyama wale walivyokuwa hawaachani watoto mbele wakubwa nyuma.Walikuwa wanakula pamoja na kuchezacheza kwa pamoja kwa kiashiria cha ishara ya upendo .

Hali ile ilimfanya Mbwa mwitu na njaa yake kuachana na jambo lake badala yake alitamani kuwa kama wao,kuishi kama wao maana alipenda sana aina ya maisha waliyonayo Digidigi 

Kwakuwa Mbwa mwitu alitamani sana maisha yale ,akaomba kuongea na kiongozi wao ili aweze kujiunga nao ili waishi pamoja.Kiongozi akamuuliza mbona hufanani na sisi?,Mbwa mwitu akasema ndiyo ila naweza jitahidi kufanana na nyinyi.Kiongozi akamwambia kapunguze mkia wako uchonge vizuri ili ufanane nasisi kisha chongesha vipembe vidogo vidogo uviweke kichwani kisha uje.Mbwa mwitu akafanya kama alivyoambiwa aliporudi kwa kiongozi, akaambiwa ondoka hapa huwezi kufanana na sisi .

Mkia wako ,miguu,kichwa na masikio bado havijaweza kufafana na sisi huna budi kutuacha.Mbwa mwitu aliondoka kwa hasira na majonzi kurudi kwa Mbwa mwitu wenzake na wao walimkataa maana tayali hafanani nao.Aliondoka akatokomea pasipojulikana huku akiwa na majonzi makubwa.

Kuna watu tunafanya vitu kama hivyo tunataka kufanana na kina fulani lakini haiwezi kuwezekana.Baki wewe kama wewe jipende jithamini na kujijali kuna upekee mkubwa upo ndani yako achana na habari za kutaka kuwa kama fulani badala yake kuwa wewe maisha yako yatakuwa bora zaidi.Tafakari chukua hatua juu ya maisha yako.

Nakukaribisha katika huduma ninazotoa ili uweze kufaidika zaidi,natoa huduma ya uandishi wa vitabu,makala na majrida huna hana ya kusema sina muda wa kuandika ninayo program nzuri ambayo itakusaidia.Program ya kubadili sauti kuwa katika maandishi hii itakusaidia sana unachotakiwa ni kuwasiliana na mimi ili uweze kujifunza zaidi 0767702659   email.maarifarobert@gamil.com Lackius Robert karibu tujifunze zaidi.

Mungu akubariki sana .

 

HATUA 6 ZA KUCHUKUA ILI KUBADILI MAISHA YAKO.

Habari za asubuhi ndugu yangu mpendwa,

 Karibu katika siku nyingine tena ambapo tunakutana katika blog yetu pendwa  yenye lengo la kukuongezea maarifa na kuifanya siku yako kuonekana mpya.

Napoleon Hill aliwahi kusema"Kuna sifa moja ambayo mtu anayependa  kushinda anapaswa kuwa nayo , nayo ni kuweka kusudi  na ujuzi wa kile kitu ambacho ana hamu ya kukifanikisha. ”.Hapa chini nimejaribu kukushirikisha maambo hatua kadhaa za kuchukua kutoka kwenye maarifa niliyoyapata kwenye kitabu cha Eat that Frog chake Brian Trace.

Katika kitabu hicho anaelezea jinsi unavyopaswa kumaliza kazi zako kwa wakati huku akitumia neno chura kama kazi yako.Anasema kabla ya kuamua kumla "chura" wako ili uendelee na kazi, lazima uamue unataka kufikia wapi kwenye  maisha yako.Utafiti unaonesha kuwa asilimia 3% ya walioweka malengo ndio waliofanikisha na wengine asilimia 97% walishindwa kuyafanikisha. Kuna hatua zifuatazo unapaswa  kuzizingatia :

1.Amua unataka uwe nani ,kaa chini tafakari chagua eneo ambalo unaona linakufaa lifanyie kazi.''kabla hujaamza kupanda ngazi ya mafanikio hakikisha ,ngazi imeninginia katika sehemu sahihi ya jengo".Lengo ni kukusaidia kufika salama katika safari yako.

2.Andika sehemu.Chukua kipande cha karatasi andika malengo yako ,wakati unaandika hakikisha unaandika malengo ambayo yanaweza kutimizika.kosa kubwa tunalofanya wengi ni kuandika malengo ambayo yapo nje ya uwezo wetu mfano mtu hana hata baiskeli anasema ninataka kununua Ndege yaani Aeroplane hiyo inakuwa ni ngumu.Kwanza kipato chako,kazi unayofanya inawezekana hairuhusu kuipata mpaka utakapokufa.Inapendeza uweke lengo ambalo unaamini ndani ya muda fulani utalitimiza.

3.Weka ukomo wa malengo yako.Maamuzi au malengo yasiyo na ukomo yanakuwa hayana uharaka ,hivyo unapopanga malengo hakikisha yanakuwa na ukomo ili kuepusha kughairisha mara kwa mara.Pia ukomo huo utakusaidia sana katika kukupa hamasa ya ufanyaji wa kazi hiyo ili uimalize kwa wakati.

4.Andika vitu vyote ambavyo unahisi ukiwa navyo vinaweza kukusaidia kuyafikia malengo yako.Hili ni muhimu maana linakusaidia wewe kuweza kuhakikisha unaweka sawa na kuwa na utayali mkubwa katika kufanya kitu hicho.

5. Pangilia vizuri mahitaji yako,weka vipaumbele/ pangilia vitu vya msingi na uenende navyo.

6. Chukua hatua.Hapa unashauriwa kufanya chochote, kumbuka "mpango wa wastani uliotekelezwa kwa nguvu ni bora zaidi kuliko mipango mingi  ambayo hakuna kitu kilichofanyika". 

Naamini lipo jambo utalichukua na kulifanyia kazi.
Wish you all the best mungu akubariki.Tuwasiliane zaidi 0767702659 Lackius Robert

Wednesday, November 04, 2020

USISHINDWE KUKAMILISHA REPORT AU KITABU CHAKO TIBA KAMILI HII HAPA.

 Habari ndugu yangu mpendwa ni matumaini yangu uanendelea vizuri na utendaji kazi wako wa kila siku,siku ya leo ninayo furaha kubwa ya kukutangazia huduma ninazotoa ni matumaini yangu utaweza kuguswa kwa namna moja au nyingine.

Lackius Robert ni kijana wa kitanzania aliyedhamilia kuleta mapinduzi makubwa hasa hasa kwenye eneo zima linaohusu fikra na mawazo chini ya program ya “Transorming the Idea” ambayo inahusika na uandishi pamoja na ufundishaji.Ambapo kupitia program hiyo unapata huduma zifuatazao 


1.  1. Ninatoa huduma ya tasfri(Translation) kutumia lugha ya Kiswahili na Kiingreza hii inawasaidia ambao wameandika vitabu ,makala,majarida na wanataka yawekwe katika moja ya lugha tajwa.

Kupitia huduma hii nimekuwa nafanya uchambuzi wa vitabu kutumia lugha ya kiswahili kwa hiyo huna haja ya kuendelea kulalamika au kusema huju namna ya kupangilia vitu vya muhimu katia usomaji wako wa viatbu tayali huduma hivyo ninaitoa kwa bei nafuu.Unaweza kubonyza link kujiunga na grup letu la telegram ili uendelee kujifunza zaidi https://t.me/SOMAONLINETELEGRAM

2.     2. Kuhifadhi nyaraka ambazo wazungumzaji( speakers ) wanakuwa wamefundisha katika semina mbali mbali.Hii inawasaidia wale ambao hawaja weza kuhudhulia semina hiyo kushiriki kwa njia ya usomaji.Kwa hiyo unapokuwa umeandaa semina yako hakun aunachopoteza mafunzo yaliyotolewa yanaendelea kuwepo na yanaweza kutimiwa kama testimony.

3.      3.  Kubadili (sound) maneno na kuyaweka katika (word) maandishi yaani transcription ambapo unapata document ikiwa katika manual transcript.Hii inawasaidia sana watu wanaohitaji kuandika vitu mbali mbali lakini wanakosa muda wa kuandika vitu hivyo inaweza kuwa ni report za kazini,vitabu au makala.Ambapo unanitumia voice note au audio mimi ninachofanya ni kuiweka katika maandishi.

4.      4.  Pia natoa huduma ya kundaa report au kuandika majina kwenye excel hii sana sana inatumika kwa watu ambao wapo bize sana kiasi kwamba wanakosa muda wa kukaa na kuandaa report au kuingiza majina hayo kwenye document husika.

5.       5. Ninatoa mafundisho katika nyanja za ushawishi,ufanisi,conflict management,malengo na maswala mazima ya kujitambua(self awereness) lakini ninaweza kubadilika kuendana na huduma anahitaji mhusika.

Huduma zote hizi hazihitaji mimi na wewe tukutane live /ana kwa ana kila siku mara nyingi zinatumika kwa njia ya mtandao unaweza kupata huduma hizi popote pale ulipo kwa bei nafuu.Njia ya mawasiliano ni WhatsApp ,Email au telegram tuwasiliane zaidi 0767702659 au email  maarifarobert@gmail.com

Karibu sana na mwenyezi mungu akubariki.


KANUNI YA P6 NA FAIDA ZAKE.

Tumia kanuni ya "P6".

Habari ndugu yangu mpendwa,natumaini unaendelea vizuri na kazi zako,karibu katika mwendelezo wa masomo yanayolenga kukupa maarifa zaidi ili uweze kusogea mbele katika maisha yako ya kila siku.Leo hii tunaenda kupata somo kidogo kuhusu kanuni ya P6 ambayo wataalamu wengi wanapenda sana kuitumia katika kazi zao ,kanuni hii imekuwa na matokeo chanya kwao karibu ujifunze zaidi.

Kanuni hii inasema Proper Prior Planning Prevents Poor Performance maana yake ni  "Mipango sahihi ya awali huzuia utendaji mbovu" unachohitaji ni kalamu na karatasi, mambo yote kuyaweka katika  orodha ya kufanya kwa  siku. Hata kama kuna jambo linaongezeka liongeze katika orodha hiyo,itakusaidia kupima na kujua nini umekamilisha na kipi bado hujakamilisha. Pia inakusaidia kutathimini maendeleo yako na kukuhamasisha kusonga mbele zaidi katika utendaji wako wa kazi.

Jambo jingine linalosisitizwa ni matumizi ya kanuni ya 10/90 wanayotumia watu makini zaidi. Kanuni hii inamaanisha kuwa kama utatumia asilimia 10 %ya muda wako katika kuweka mipango na kupangilia kazi yako kabla hujaanza, utaokoa asilimia 90% ya muda wa kufanya kazi ukishakuwa umeanza. Alex Mackenzie aliwahi kusema ’’ mipango bila vitendo ni mwanzo wa kushindwa’’.

Hivyo basi kila jambo unalotaka kulifanya lazima utilie mkazo katika mipango kila jukumu au shughuli unayotaka kuifanya kwa siku fulani lazima uiwekee muda maalumu wa kujiandaa. Ujue utafainyaje, wakati gani, kwa rasilimali zipi, ni akina nani utafanya nao, nani atafanya nini, muda gani?.Chukua hatua juu ya maisha yako maana wewe ndiye dereva mkuu wala hakuna mtu mwingine.

Naamini kuna jambo umejifunza karibu tuendelee kujifunza zaidi kupitia program zangu za usomaji wa vitabu ambazo ninazifanya kutumi lugha ya kiswahili,Tuwasiliane zaidi mimi ni Lackius Robert 0767702659 au email maarifarobert@gamil.com. au bonyeza link ya telegram uweze kupata vitabu zaidi   https://t.me/SOMAONLINETELEGRAM .
Karibu tujifunze zaidi na mungu akubariki.

 






Tuesday, November 03, 2020

HATUA KADHAA ZA KUKUWEZESHA KUWA NA MAISHA BORA.

 HATUA KADHAA ZA KUKUWEZESHA KUWA NA MAISHA BORA KUTOKANA NA UCHAMBUZI WA DR.MAKIRITA AMANI.

 VOLUME 1.CHUKUA HATUA

Ø  -Tengeneza akili ya kibilionea. Huwezi kuwa na maisha mazuri kama huna maarifa mazuri unayoingiza kwenye akili yako. Jifunze kila siku kwa kusoma vitabu, kuhudhuria semina na mikutano, kuangalia video, kusikiliza vitabu na kila fursa inayojitokeza mbele yako ya kujifunza.

Ø  -Tengeneza mageuzi yanayokuwezesha kufanikiwa. Charles Darwin aligundua kwamba, viumbe hai wenye nguvu ndiyo walioweza kuishi na kuzaliana, wale waliokuwa dhaifu walikufa. Ili uweze kuwa na maisha mazuri, lazima uweze kutengeneza mageuzi ambayo yatakuwezesha kuendelea kuwepo wakati wote. Uwe tayari kubadilika, usibaki pale ulipo wakati wote.

Ø  -Kuwa mnyenyekevu. Jua kwamba huwezi kujua kila kitu, unahitaji msaada wa wengine kufanikiwa.
Ø  Kuwa na mtu/watu ambaye unamwangalia na anakuhamasisha kuchukua hatua. Watu hawa wanaitwa mamenta, ni watu ambao watakuwezesha kupiga hatua kubwa zaidi ya ulipo sasa.
Ø  Tofauti ya watu masikini na matajiri ni nidhamu. Wote wanapata fedha, matajiri wana nidhamu ya kudhibiti matumizi, kuweka akiba na kuwekeza. Masikini wanatumia fedha yote mpaka iishe, na wanaenda kukopa.

Ø  -Ondokana na mawazo ya bahati nasibu/kamari. Hakuna kitu kizuri kinachotokea kwa bahati na kwa haraka au njia ya mkato. Wapo ambao wamekuwa wakifikiria wanahitaji kushinda bahati nasibu au kamari ili wafanikiwe, dunia haifanyi kazi hivyo. Hata wanaoshinda bahati nasibu au kamari, haiwachukui muda, wanarudi kwenye umasikini.

Ø  -Ondokana na hali ya kuona kwamba huwezi. Tumefundishwa woga na kuona peke yetu hatuwezi, mpaka tufanyiwe kile ambacho wengine wamekuwa wanatufanyia. Unahitaji kuondokana na hali hiyo, na kujua kwamba una uwezo mkubwa wa kufanya makubwa. Utumie.

Ø  Usizichukie jumatatu na kuzipenda ijumaa. Kwa maisha ya mafanikio, siku zote zinapaswa kuwa sawa. Lakini wasio na mafanikio, huchukia jumatatu na kuziita blue Monday na kuzipenda ijumaa na kuziita TGI (Thank God It’s Friday). Fanya kile unachopenda, ambacho utakifanya kila siku ya maisha yako.

Ø - Unaweza kusoma kitabu kimoja kila siku. Kusoma vitabu ni njia ya kutengeneza timu yako ya washauri kwenye kila unachofanya. Tai Lopez amekuwa na utaratibu wa kusoma kitabu kimoja kila siku, kwa kutafuta yale maarifa muhimu ya kitabu na kukazana na hayo. Anasema vitabu vingi vina maelezo mengi ambayo huyahitaji, ukishajua unataka nini, ni rahisi kusoma vitabu vingi.

Ø  -Kugeuza makaa kuwa almasi. Almasi ndiyo kitu kigumu kuliko vitu vyote duniani, lakini inatengenezwa na makaa ambayo siyo magumu sana. kinachotokea ni makaa hayo kuwekwa kwenye presha kubwa mpaka yanakuwa almasi. Hivyo kama wewe unataka kuwa almasi, lazima upitie mazingira magumu, yanayokutengeneza na kukufanya kuwa bora zaidi.

Ø - Jiandae kwa matokeo mabaya, lakini tegemea matokeo mazuri. Mara nyingi mambo hutokea kwenye maisha na kujikuta hatujajiandaa. Hii ni kwa sababu huwa tunafikiri kila kitu kitaenda kama tunavyotaka. Ukweli ni kwamba mambo hayaendi kama tunavyotaka sisi, bali yanaenda kama yanavyoenda yenyewe. Hivyo ni muhimu ujiandae kwenye lolote unalofanya, ili matokeo yakija mabaya, uwe na maandalizi, na yakija mazuri, ufurahie.

Ø  -Nguvu za asili. Jua kwamba kuna nguvu za asili, ambazo huwezi kuzivunja na ukabaki salama. Kama ambavyo ukipanda kwenye jengo refu na kujiachia lazima uanguke chini na uumie, japo ndege hawaumii kwa kufanya hivyo. Kila unachofanya, usilazimishe mambo ambayo yatakwenda kinyume na nguvu za asili. Mfano usitake kuanza biashara leo halafu kesho ikawa ina mafanikio makubwa, kila kitu kinachukua muda.

Ø  -Tengeneza mfumo bora wa kupanga mambo yako. Kupanga kuna faida kuliko kutokupanga. Lakini kupanga pekee hakuna msaada mkubwa. Unahitaji kuwa na mfumo wa mipango, ambapo unakuwa na mpango zaidi ya mmoja. Unakuwa na mpango wa mambo yakienda vizuri, unakuwa na mpango wa mambo yakienda vibaya, halafu unakuwa na mpango wa mambo yanavyoweza kwenda. Kwa kuwa na mipango hiyo mitatu, hutakwama pale mambo yanavyokwenda tofauti na ulivyotegemea.

Ø  -Tengeneza kundi la kukusaidia kufanikiwa. Hakuna mtu anaweza kufanikiwa kwa nguvu zake yeye mwenyewe, kila mtu anahitaji msaada wa watu wengi ili kuweza kupiga hatua kubwa. Unahitaji kuwa na kundi la watu ambao unawategemea na wanakusaidia kupiga hatua. Unahitaji kuwa na marafiki ambao wanakupa hamasa ya kupiga hatua na kukushauri vizuri. Unahitaji kuwa na kundi la washauri (mastermind) ambao wanakufuatilia kwa karibu kwa kila unachofanya. Pia unahitaji wasaidizi kwenye yale unayofanya.

Ø  -Zima ujinga wako. Watu wengi hufikiri wanajua sana kumbe hata hawajui, wengine wanaamini wapo sahihi zaidi kumbe hawapo sahihi. Ili uweze kujifunza, lazima ukubali kuzima ujinga wako. Lazima ukubali kwamba hujui ndiyo ujifunze, lazima ukubali kwamba huenda unakosea ili uwe sahihi. 
Ukiamini unajua na uko sahihi mara zote, utakuwa na ujinga wako milele.

Ø  -Kuwa mmoja kati ya mia moja. Allen Nation aliwahi kunukuliwa kusema siri ya mafanikio kwenye maisha ni kuwapuuza watu 99 kati ya watu 100 na kumsikiliza mtu mmoja. Tafuta yule anayekufaa, yule anayejua na anayekupa hamasa ya kupiga hatua, na msikilize huyo, wapuuze wengine kwa sababu huna muda, fedha wala nguvu za kumsikiliza kila mtu. Kwa upande wa pili, wewe pia unahitaji kuwa mmoja kati ya 100 wanaofanya kile unachofanya wewe, ukifanye kwa ubora na tofauti kubwa sana.

Ø  -Chagua eneo dogo unaloweza kulitumikia vizuri. Watu wengi wamekuwa wakifikiria kuanza na eneo kubwa, kuhudumia kila mtu na kuishia kushindwa kabisa. Chochote unachotaka kufanya, anza kulenga eneo dogo, chagua kikundi cha watu ambao utawatumikia vizuri, ambacho utatawala kwa kile unachofanya, na hapo utatengeneza mafanikio makubwa kuliko kutaka kumfikia kila mtu.

Ø  -Tengeneza makosa madogo na Kila mtu anakosea kwenye maisha, lakini kukosea kwenye mambo madogo na machache, kunakuwezesha kujifunza na kutokurudia makosa hayo. Kukosea kwenye mambo makubwa na mengi, kunaweza kukuondoa kabisa kwenye safari ya mafanikio. Kwa mfano kama hujawahi kuanza biashara kabisa si vyema kuchukua mkopo mkubwa na kwenda kuanza biashara, utakosea halafu utapata hasara kubwa. Badala yake unahitaji kuanza na biashara ndogo na kukua, utajifunza kupitia makosa madogo utakayofanya, ambayo hayataua kabisa biashara yako.

Ø  -Nguvu ya mawasiliano. Siyo unachosema, bali unakisemaje ndiyo kina nguvu. Unahitaji kutengeneza mawasiliano yenye nguvu, ambayo yatakuwezesha kufikisha ujumbe wowote ambao unataka uwafikie watu na waweze kuchukua hatua. Unapotoa ujumbe, wafikirie wale unaowapa ujumbe, na jua kitu gani kinawahamasisha kuchukua hatua. Kwa kujua hayo, utaweza kuwahamasisha kuchukua hatua.

Ø  Kila mtu ashinde au usikubaliane kabisa. Kuna aina tatu za makubaliano, moja mmoja ashinde na mwingine ashindwe, mbili, wote washinde, tatu wote washindwe. Unapoingia kwenye makubaliano yoyote na mtu yeyote, hakikisha kila upande unashinda, kama hilo haliwezekani basi ondoka kwenye makubaliano hayo, hata kama wewe unashinda na upande mwingine unashindwa. Njia pekee ya kujijengea sifa bora na ushirikiano na wengine, ni kumwezesha kila mtu anayejihusisha na wewe kushinda.

NI Nimatumaini yangu makubwa kuwa kuna kitu umeweza kujifunza ,karibu upate uchambuzi wa vitabu kwa lugha ya kiswahili tena kwa bei nafuu vitabu kama Rich dad poor dad,think and grow rich na vitabu vingine kadha wa kadha tayali tumevichambua tayali tuwasiliane kupitia 0767702659 Lackius Robert au bonyeza link kujiunga katika kundi letu la telegram 


MMungu akubariki zaidi.
N

USIKATE TAMAA,Hadithi ya Chura.

 

Karibu ndugu yangu mpendwa upate kuijua zaidi hadithi ya Chura kiziwi lipo jambo utaweza kujifunza.

Ndugu ,

Walikuwepo Vyura waliokuwa wakisafikiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine gafra vyura wawili kutoka katika kundi hilo wakaanguka shimoni.Wenzao walipoangalia urefu wa shimo lile wakawa wanashangilia kwa kuwambia msijisumbue kutoka humo maana shimo ni kubwa ,kubali tu kufa amna namnana ya kujitoa.

Waliobaki juu walianza kuwashangilia huku wakiwaambia acheni kujisumbue eti kuruka kutoka katika shimo hilo ,kubali tu kufa.

Mmoja akakubali kukata tamaa mwishowe akafa akiwa katika shimo hilo.Mwingine akazidi kujitahidi kuluka ili ajitoe katika shimo ,mwishowe akabahatika kujitoa.

Wenzake wakaanza kushangaa kwa jinsi alivyoweza kujitoa katika shimo lile,Kumbe chura yule alikuwa ni kiziwi hivyo hakuwa anasikia waliyokuwa wanasema badala yake alijua wanakazana kumshangilia kwa jitihada anazofanya kujiokoa.

Katika maisha yetu ya kila siku kuna wakati tunahitaji ukiziwi fulani hivi ili mambo yaende wakati ,wengine wanakazana kukukatisha tamaa wewe songa mbele ,ukiwasikia mazuri hutoyafikia utaishia njiani.

Tafakari Chukua hatua juu ya maisha yako.Wish you all the best.

Mimi ni Lackius Robert karibu katika program yetu ya usomaji wa vitabu ambapo tunachambua vitabu kwa lugha ya kiswahili bonyeza link kujiunga katika grup letu la telegram  https://t.me/SOMAONLINETELEGRAM  .

Karibu tujifunze zaidi vitabu vyote tunavichambua kwa lugha ya kiswahili au tuwasiliane zaidi kupitia 0767702659 mungu akubariki zaidi.

MAKALA YA EMOTIONAL INTELLIGENCE

MAKALA YA EMOTIONAL INTELLIGENCE KUTOKA KATIKA MAANDISHI YA WATU TOFAUTI TOFAUTI.

Maana kubwa ya emotional intelligence ni kuelewa na kuthibiti hisia zako ili uweze kukabiliana na mazingira yanayokukayokuzunguka.

Watu wengi wanaweza kuanzisha mahusiano lakini siyo kila mmoja anaweza kuendelea nayo katika hali ya amani n afuraha wapo wanaoishia katikati kutokana na kukosea katika vitu fulani fulani.

Tafiti nyingi zinaonesha watu wenye akili nyingi au IQ kubwa Ndio wanaweza kufanikiwa lakini zimekuja na usemi kwamba kuwa na akili nyingi haitoshi bali unatakiwa kuwa na uwezo wa kuthibiti hisia ambazo zinaitwa EQ emotional QuotentI akili ya utambuzi,au Emotional Intelligence akili hisia .

Jinsi ya kuboresha mahusiano yako kwa kutumia Emotioanal intelligence kuna hatua nne ambazo ni vema kuzijua ili uweze kuyaboresha zaidi kama nilivyoelezea hapa chini;

Hatua ya kwanza (Self management) Namna ambavyo wewe unaweza kuthibiti hisia zako ,Mfano unapokuwa na hisia za hasira ,kuvurugwa ,kukataliwa,kukatishwa tamaa,mtu kukusemea kitu ambacho hujafanya unawezaje kuthibiti hisia hizo?.

Ata kama una akili nyingi,vipaji vingi sana ukishindwa kuthibiti hisia zako hutoweza kufika mbali.Mara nyingi tunasema unapokuwa umekasirika sana ili usifanye mambo mabaya unatakiwa uwe na uwezo wa kujizuia licha ya hasira inayokusonga.Kama huwezi kumiliki na kutawala hisia zako huwezi kufika mbali katika maisha yako maana kila wakati utakuwa unagombana na watu.

Hatua ya pili (Self awereness )Namna unavyojitambua,kutambua nguvu ulizonazo kihisia,namna ya kutambua udhaifu ulionao kihisia.

Hii ni nzuri kufahamu maana inakusaidia katika kufanya chaguo kulingana na ubora na udhaifu wako.Kuna watu ambao wakishakuwa na hasira au kukwazwa wakiongea lazima wavuruge,lakini ukiwa unatambua nguvu iliyo katika hisia zako pindi ukiwa na hali fulani itakusaidia kuongea vizuri na watu.Kama una hasira unaweza kunyamaza ili usilete vurugu au kuharibu mipango ya watu,kuna wakati unatakiwa kunyamaza siyo kwamba huna cha kusema ila unaogopa kuharibu mahusiano.Kumbuka unaweza kusema neno moja tu likaharibu mahusiano yako na watu tena uliyojenga kwa muda mrefu.

Hatua ya  tatu ni (social awereness)Namna ambavyo unaweza kuchukulia hisia za wengine ,kuthibitbiti hisia zao,uwezo wa kutambua hisia za watu wengine.

Kujua kwa nini mtu fulani anakuwa na hisia za fulani labda hasira au furaha ni vizuri maana utaweza kuongea naye na kumshauri pia uku ukizingatia hisia alizonazo.Ili uweze kufanikiwa unatakiwa kujua namna ya kuenenda na hisia za watu wengine ili uweze kuendana nao vizuri.Kuna wakati unaweza kutamka neno kwako likawa zuri lakini kwa wengine likawa linawakera au kuwabadilisha hali yao kihisia na kuwaletea shida.

Fahamu,jali na uthibiti hisia za watu wengine.

Hatua ya nne(Relationship management) Uwezo wako wewe kuhusiana na watu.

Wezo huu umegawanyika katika sehemu tatu

i.Namna ya kujenga mahusiano

ii.Namna ya kudumisha mahusiano.

iii. Namna ya kukabiliana na mogogoro  tofauti inayokuwa inatokea katika mahusiano .Ukiweza mambo haya matatu mahusiano yako na wengine yatakuwa mazuri.

Ukishindwa kufatria hatua hizi nne nilizoainisha bila kujali una maono kiasi gani,malengo,vipaji na uelewa kiasi gani hutoweza kufanikiwa katika maisha yako hasa hasa eneo lako la hisia.

Pia hapa kuna mwendelzo wa namna ya kutumia emotional intelligence kwa watu wa karibu;

-# Kitu kinachomtofautisha binadamu na mnyama ni uwezo wa kufikiri.

Binadamu ana utashi,ana uwezo wa kufikiri,kuamua na kufanya maamuzi sahihi. Kitu kinachomfanya binadamu awe binadamu ni kufikiri. Kufikiri ndio kazi ya binadamu na hiyo ndiyo inayofanya emotional inetelligence yako kuwa kubwa zaidi.

Ndiyo maana kabla ya kuongea binadamu anatumia muda kufikiri. Kufikiri kunaongeza umakini kitu cha kuongea ili kiweze kumfikia mhusika vizuri.

Karibu upate huduma hizi -program za usomaji wa vitabu ambapo kuna huduma ya SOMA ONLINE WhatsApp na Telegram huduma hizi ni bure na huduma ya NDANI YA KITABU hii channel ipo telegram tu ambapo ina mkusanyiko wa vitabu vinne kila mwezi kwa gharama ya sh.5000/=

1.      - Ninatoa huduma ya tasfri(Translation) kutumia lugha ya Kiswahili na kiingereza hii inawasaidia ambao wameandika vitabu ,makala,majarida na wanataka yawekwe katika moja ya lugha tajwa.

2.       Kuhifadhi nyaraka ambazo wazungumzaji( speakers ) wanakuwa wamefundisha katika semina mbali mbali.Hii inawasaidia wale ambao hawajaweza kuhudhulia semina hiyo kushiriki kwa njia ya usomaji.Kwa hiyo unapokuwa umeandaa semina yako hakuna unachopoteza mafunzo yaliyotolewa yanaendelea kuwepo na yanaweza kutumiwa kama testimony.

3.      -Kubadili (sound) maneno na kuyaweka katika (word) maandishi yaani transcription ambapo unapata document ikiwa katika manual transcript.Hii inawasaidia sana watu wanaohitaji kuandika vitu mbali mbali lakini wanakosa muda wa kuandika vitu hivyo inaweza kuwa ni report za kazini,vitabu au makala.Ambapo unanitumia voice note au audio mimi ninachofanya ni kuiweka katika maandishi.

4.      -Pia natoa huduma ya kundaa report au kuandika majina kwenye excel hii sana sana inatumika kwa watu ambao wapo bize sana kiasi kwamba wanakosa muda wa kukaa na kuandaa report au kuingiza majina hayo kwenye document husika.

5.     - Ninatoa mafundisho katika nyanja za ushawishi,ufanisi, conflict management,malengo na maswala mazima ya kujitambua(self awereness) pia naweza kubadilika kuendana na aina ya mfundisho ambayo mhusika anataka yatolewe

kukuna huduma zinazohitaji tuonane na kuna ambazo hazihitaji mimi na wewe tukutane live /ana kwa ana zote zinatumika kwa njia ya mtandao unaweza kupata huduma hizi popote pale ulipo kwa bei nafuu.Njia ya mawasiliano ni WhatsApp , Email au telegram tuwasiliane zaidi 0767702659 au email  maarifarobert@gmail.com au bonyeza link hii kujiunga na gruop letu la telegram  https://t.me/SOMAONLINETELEGRAM  .

Karibu sana na mwenyezi mungu akubariki.