Napoleon Hill kwenye kitabu chake cha "Think and Grow Rich" anasema "washindi kwamwe hawaachi kufanya".
Hii kauli inatosha kukupa nguvu na imani kuwa unaweza kuwa mshindi katika mchezo wowote. Iwe mpira, biashara, muziki au kitu kingine.
Ikiwa unacheza mpira, kama utaendelea kufanya mazoezi bila kuacha. Kujifunza mbinu mpya na kuwa na nidhamu bora hakuna namna utashindwa kufunga magoli mengi zaidi.
Upo kwenye biashara, ushindi wako ni mauzo. Maana kupitia mauzo ndipo pesa hupatikana. Ushindi huo unaenda kuupata pale ambapo utaamua kufanya endelevu bila kuacha. Unajifunza mbinu mpya za masoko kila siku. Hapo lazima uuze na mchezo wa mauzo kwako itakuwa raha maana utakuwa ni mshindi.
Upo kazini, ikiwa utaonyesha kujali, kujituma, kuwa na nidhamu na kumaliza kazi kwa wakati. Lazima uwe mshindi katika kazi zako. Maana kupitia nidhamu utajiboresha na kukamilisha kazi zako kwa muda muafaka.
Ushindi ninaozungumza hapa sio tu wa goli kusema wachezaji ndio wanaostahili kushinda la asha! Ni ushindi katika kazi zako.
Hawajibu message piga simu. Hawajapokea simu watembelee. Mara zote hakikisha kuna kitu kikubwa unakifanya ukilinganisha na hapo awali.
Mwanamziki piga kazi zaidi. Jifunze na andaa muziki wenye maadili ili watu wote waweze kupata ujumbe. Kuwa mvumilivu usikate tamaa haraka sana. Ushindi kwenye mziki ni wako. Endelea kuonyesha juhudi kubwa.
Changamoto ni nyingi tunapitia, wewe fanya tu, timiza wajibu wako kufanya. Kama ni simu 20 wewe piga, kama ni kuwatembelea watu 10 kwa siku ili uwauzie wewe nenda. Kama ni mazoezi wewe nenda.
Hakikisha mara zote, unakuwa kazini. Fanya bila kuchoka. Unaambiwa mchumia juani ulia kivulini. Wakati ndio huu ushindi wako unakaribia. Kila lakheri.
Je, ni nini kinakukwamisha ushindi wako kwenye kazi zako?
Bonga nasi hapa hapa 0767702659
Imeandaliwa na Lackius Robert
Karibu sana tujifunze zaidi.
No comments:
Post a Comment