Friday, March 17, 2023

Nini kinafanya wakuchague?


Siku moja nilialikwa na taasisi moja kwa ajili ya kusimamia zoezi la usaili wa kazi. Kwenye jopo tulikuwa watu wanne . Kwa sababu mimi ni mtaalamu katika masuala la Sheria za Kazi na Ajira. Walinipa nafasi kubwa na wote walikuwa wanasikiliza neno la mwisho kutoka kwangu. 

Usaili kiukweli ulienda vizuri, nikiwa makini sana kuhakikisha anapatikana mtu sahihi. 

Wakati tunaendelea na usaili kuna dada mmoja tumuite Mwajuma japo sio jina lake halisi aliingia akaanza kujielezea background ya elimu na ujuzi wake. 

Kikafika kipindi cha maswali nikamuuliza swali la kwanza. Je, unajua nini kinafanya tukuchague wewe? 

Mwajuma akasema, ni Kwa sababu mkinichagua nitaweza kumsaidia baba yangu anayeumwa nyumbani. Matibabu yatatokana na mshahara mtakaonilipa. 

Nilimwambia tumekusikia. Nikashika kichwa na kujiuliza maswali mengi. Je, huyu anajua anachofanya? Na hiki alichosema anakijua au amesahahu kwamba  hakuna mtu anayekupa kazi kama msaada. 

Baadaye wakata tutoe hitimisho juu ya usaili mzima. Binafsi nilimwambia bosi kwamba mtu pekee mwenye sifa alikuwa ni mmoja tu Mwajuma. Ila tatizo ni moja. Ajajua ni kwa nini anatafuta kazi. 

Kwa hiyo either mtangaze upya au mchukue Mwajuma kisha muelekeze namna bora ya kufanya kazi. Mwambie hupewi kazi kwa sababu ya matatizo uliyo nayo au kama msaada bali ujuzi na namna unavyoweza kuisaidia taasisi kuzalisha zaidi. 

Note: Ukiwa unaomba kazi mahali popote pale, elezea namna utakavyofanya kazi hiyo kwa ufanisi, uadilifu na faida utakayoongeza. Na sio unavyotaka kutatua matatizo yako kupitia kazi.

Usiseme  nina mtoto mdogo na hakuna wa kunisaidia. Ninataka kujikimu kimaisha. Baba yangu anaumwa au mama yangu au kwa sababu nipo tu nyumbani.

Waambie ninaweza kufanya 1, 2, 3 na nipo tayari kufanya kazi kwa jitihada zote ili kuhakikisha kampuni au biashara hii inafikia hatua nzuri.

Sehemu nyingi za kazi wanatafuta wafanyakazi wanaoenda kuleta suluhu na sio kuongeza matatizo. Ikiwa umepata nafasi, usiichezee tena umefika kwenye usaili wa kuongea. Hupaswi kutia doa. 

Funguka onyesha ujuzi wako, hadi wanaofanya usaili washangae. Hii itafanya waone kitu cha ziada kwako. 

Waonyeshe namna unavyoenda kukuza uzalishaji katika kampuni au taasisi husika. Itakutofautisha na wengine. 

Umewahi kukataliwa mahali kisa huna vigezo, ulijua kwa nini? 
Bonga nasi hapa hapa 

Imeandaliwa na Lackius Robert 
Hamasikaacademy2023

No comments:

Post a Comment