Tuesday, March 07, 2023

Hiki ndicho huvunja uaminifu

Ni matumaini yangu kuwa umewahi kusikia watu wakisema fulani kanichomesha mahidi au kaniacha njia panda na maneno mengine. 

Kanipa ahadi hafu kashindwa kuitimiza. Ni hali ambayo inamfanya mtu anakasirika sana. Na mwanzo mpya wa kutopokea simu ya mtu au kukata mawasiliano. 

Huenda imewahi kukutokea au haijawahi kukutokea. Ila ukweli ninaotaka uujue leo ni kuwa: hakuna kitu kinavunja uaminifu kwa mtu kama kutotimiza ahadi. 

Kuweka ahadi ni rahisi ila kazi ipo kwenye kuitimiza. Unapoweka ahadi na mtu, iwe ya pesa au zawadi, jua kuna umakini unautengeneza kwa mtu. 

Kama ni pesa ahadi yako inamfanya aweke mipango juu ya pesa hiyo. Inapotokea hujaweza kutumiza ahadi hiyo lazima mgombane. 

Kuna kitu kinapungua ndani yake ambacho ni uaminifu. Namna ambavyo alikuwa ana imani juu yako anapunguza. 

Ninaposema ahadi sio tu kwenye pesa ata maeneo mengine. Wewe kiongozi umeahidi kutekeleza vitu fulani ndani ya uongozi wako. Muda Miaka mitano inapoisha hujatekeleza. Jua kuna kitu unakipunguza kwa watu wako ambacho ni uaminifu. 

Unahitaji nini ili kutimiza ahadi? Kitu unachopaswa kujua ni kwamba. Sio usome masomo ya juu au usome vitabu 100. Unachohitaji ni uwezo wa kufikiri kilichosahihi kwa wakati sahihi. Usitoe ahadi ukiwa na FURAHA sana au UMEKASIRIKA sana. Toa ahadi ukiwa katika hali yako ya kawaida. 

Kingine, toa ahadi iliyo ndani ya uwezo wako. Epuka kutoa ahadi kwa sifa. Upo mbele za watu au kwenye harusi. Unataka watu wakuone baba la bab au mama la mama itagharimu. 

Weka ahadi iliyo ndani ya uwezo wako. Hii itakusaidia kuitimiza bila kuwa na wasiwasi. Watu wengi huweka ahadi ili wasifiwe inapofika kwenye kuitekeleza ndipo shida huanzia.

Ahadi haipaswi kuwa ile ya kukufanya ukose amani. Inapaswa kukupa hamasa kutafuta zaidi. Weka akilini kuwa, kinachovunja uaminifu ni ahadi hewa. Take care uutunze na kuulinda uaminifu. 

Je, ahadi ipi uliahidi na hukutimiza? 
Bonga nasi hapa hapa 0767702659 

Imeandaliwa na Lackius Robert 
#36mwangaza2023

No comments:

Post a Comment