Imekuwa kasumba kwa wengi wetu hasa mahali pa kazi kukwepa baadhi ya majukumu.
Wakati mwingine unaenda katika ofisi fulani, ukitaka kupewa huduma fulani. Mhusika unayekutana naye, anakwambia nenda meza ile huyo atamaliza shida yako.
Unapochukua hatua ya kwenda kwa huyo mtu uliyeelekezwa labda ni IT au customer care badala amalizie shida yako anakwambia subiri kesho au kesho kutwa kuna mfumo haupo sawa.
Pengine hamna shida yoyote, amejisikia uvivu tu. Hii hali imekuwa inarudisha nyuma maendeleo yetu kwa kiasi kikubwa.
Unaenda kwa fundi anakwambia njoo baada ya siku mbili. Ukienda anakwambia umeme ulikata njoo keshokutwa. Ukija anakwambia kuna kifaa kakiagiza mahali. Huo wote ni uvivu tu wa kufanya kitu chako.
Hii hali inapoendelea kuna watu wanaanza kujitoa taratibu taratibu kwenye biashara au huduma yako. Kwa sababu hakuna kitu wateja au watu wanakwepa kama kuzungushwa mara mbili au tatu. Ukimfanyia hivyo jua umempoteza.
Ili tuwafanye wathamini huduma zetu, tuache uvivu kama kazi imekuja kwako ifanye kwa moyo wote. Muheshimu aliyeacha kazi zake akaja kwako umfanyie kazi.
Kama ingekuwa halipi pesa yake sawa. Lakini wanalipa pesa ndicho kinachoumiza moyo. Pesa inatafutwa kwa shida. Hivyo, ukiiheshimu na ukaipokea kihalali watakuheshimu na kukupa kazi nyingi.
Lijue hili likusaidie kukuza brand yako. Acha uvivu fanya kile kinachowezekana.
Una changamoto yoyote bonga nasi hapa hapa 0767702659
Imeandaliwa na Lackius Robert
Hamasika 2023
No comments:
Post a Comment