Thursday, March 02, 2023

Jifunze Ushirikishe

Ukweli ni kuwa kila mmoja wetu kipo kitu anakijua zaidi wengine. Huenda ni upande wa hesabu, lugha, fedha, uongozi, mahusiano au biashara. 

Kila wakati umekuwa mstari wa mbele kujifunza vitu vipya. Lakini cha kushangaza kuna baadhi ya vitu umekuwa ukivisahau. Hali inayokufanya kurudia kuvisoma tena ili vikae. 

Hali hii ya kuwa unasahau kuna wakati imekuwa ikikunyima furaha. Kwa sababu muda ambao ungefanya kitu kingine unautumia tena kupitia. 

Umekuwa unajiuliza namna ipi nzuri kujenga kumbukumbu ya muda mrefu. Njia hii hapa "jifunze shirikisha". 

Ipo hivi "you learn best when you teach another" kwa lugha nyepesi. Unajifunza kuwa bora kupitia kufundisha wengine. Hii ndiyo siri ninayokupa leo. 

Unasoma masuala ya ndoa. Unasoma makala na vitabu vya ujasiriamali, sanaa, biashara au uongozi. Tafuta sehemu au watu wa kushirikisha maarifa yako. 

Inaweza kuwa katika mitandao ya kijamii kama Facebook, Whatsapp, linked au telegram. Au ukaamua kuandika kitabu au jarida, linaloelezea masuala mbalimbali unayojua. 

Uzuri wa kushirikisha ni kwamba unapata uelewa zaidi. Tunasema unachomfundisha mtu kinanasa haraka akilini kuliko kile usichoshirikisha. 

Jifanyie tathmini. Hata kama ni vitu vya kawaida kama kumfundisha mtu kutumia simu, kupika chakula fulani. Namna unavyokumbula hatua zote. Na pengine unahisi kama yule uliyekuwa unamfundisha upo unamuona mbele yako. 

Wenye uwezo mzuri wa kutunza kumbukumbu hawajashushwa kama ulivyokuwa unadhania. Walichukua wajibu kujifunza na kushirikisha yale wanayojua. 

Wakati ndio huu. Ifanye dunia ijue kile kilichomo ndani yako. Ili baadaye uwe na uwezo mkubwa kuwa na kumbukumbu nzuri. 

Je, nini kilikuwa kinakukwamisha kuweka kumbukumbu zako? 

Bonga nasi hapa hapa 0767702659 

Imeandaliwa na Lackius Robert 
#32mwangaza2023

No comments:

Post a Comment