Saturday, March 04, 2023

Hii ndiyo sababu inayofanya usahau ulichojifunza

Mara ngapi umekuwa unajifunza vitu vingi na kutofanyia kazi hata kimoja? 

Unakumbuka ile siku uliyomaliza kusoma kitabu fulani? Ule mzuka uliotoka nao ukasema nitaenda kufanyia kazi kile ulichojifunza. Ila baada ya siku kadhaa kupita hakuna kilichofanyika. 

Au ulipotoka kwenye semina ya biashara, uongozi, mahusiano au ndoa. Uliwahakikishia watu kuwa unaenda kufanya mabadiliko makubwa sio tu katika kazi zako bali katika maisha yako. 

Kila walipokuuliza uliwaambia umejifunza mambo mengi sana, kiasi kwamba unaenda kufanya maajabu makubwa. Mwezi mmoja mbele hamna kilichofanyika. Umesahau kila kitu. Unataka kujua tatizo ni nini? 

Ipo hivi "To know and not to do, is really not to know. To learn and not to do is not to learn". Kwa lugha nyepesi; kujua kitu na kutokifanya ni sawa na kutokijua. Kujifunza kitu na kutokifanyia kazi ni sawa na kutojifunza. 

Huu ndio ukweli. Unaweza kujifunza vitu vingi lakini ukachagua vile vichache vya kufanyia kazi. Mfano unaposoma kitabu usijipe presha et hadi ufanyie kila kitu. Chagua vitu vichache vya kufanyia kazi. 

Umehudhuria semina, umejifunza mengi. Huwezi kuyafanyia kazi yote chagua machache ya msingi. Umejifunza kuwa, ili uweze kuwa mwekezaji lazima utunze asilimia 30 ya kipato chako, asilimia 10 ya zaka au kumshukuru Mungu. Asilimia 10 msaada au asilimia 50 ya matumizi kwa mfano. Huwezi kuanza vyote kwa pamoja. 

Anza kidogo kidogo na kitu kimoja. Ili baadaye uanze kuzoea. Ila usipofanyia kazi vitu vyote. Jua ni sawa na kutojifunza. Utaelewa zaidi baada ya kuanza kufanyia kazi kitu. 

Mmejifunza biashara. Ili upate ufahamu mzuri wa biashara, fungua biashara. Hapo ndipo utaanza kuona namna gani mambo yanavyoenda na hapo ndipo utapima ubora na uelewa wako, kuhusu mliyojifunza. 

Kila siku, jifunze kitu na ujenge utamaduni wa kufanyia kazi machache uliyojifunza. Itakusaidia kwa kiasi kikubwa kuelewa na kukumbuka zaidi. Ndiyo maana unasahau kile ulichojifunza kwa sababu hufanyii kazi kitu hicho.

Je, ni nini kinakukwamisha kufanyia kazi uliyojifunza? 

Bonga nasi 0767702659 
Lackius Robert 
#33mwangaza2023

No comments:

Post a Comment