Saturday, March 11, 2023

Mabadiliko yanaanza na wewe


Kama kitu kimetengenezwa kinaweza kubadilishwa. Kama kitu kina uhai kinaweza kubadilika kwa hali fulani fulani. 

Chukulia mtoto mdogo anapozaliwa, haanzi kuongea, kutembea au kuwa na meno. Kadiri muda unavyokuwa unasogea ndivyo anavyokuwa anabadilika mdogo mdogo. 

Chukulia mti wa Mbuyu, mwanzoni huwa unaanza kama mchicha. Wakati huo umbo likiwa dogo sana kadiri muda unavyokuwa usogea ndivyo hubadilika pia. Hadi kuwa na umbo kubwa. Ukiambiwa ulikuwa katika umbo dogo unaweza usikubali lakini huo ndio ukweli. 

Ipo hivyo kwenye maisha yako. Hutaweza kubadili mwili au kujiongezea kiungo kingine kwa maana ya mkono wa watatu au mguu wa tatu la asha! Namaanisha unaweza kuibadili hali ya sasa kuwa bora zaidi. 

Huwezi kuibadili jana ila unaweza kuitumia leo kuiboresha kesho yako. Mabadiliko yote haya yanaanza na wewe mwenyewe. Kukubali kuwa kuna mahali unataka kufika. Kuna kitu unataka kukipata katika maisha yako. Kuna hatua kubwa unataka kuipiga. 

Huo ndio ukweli ninaotaka uweze kuujua "any changes starts with you" mabadiliko yoyote yanaanza na wewe. 

Unataka kubadilika kifikra, kimawazo, kimtazamo na kihisia pia. Hii itakusaidia kuwa tayari kutimiza wajibu wako. Kumaliza kile ulichokianza, bila kujali ugumu kiasi gani unapitia. 

Matumaini unayotaka kuwa nayo. Kuwa tayari kupata habari zaidi. Usipoamua kufanya kitu tambua kuwa wewe ndiye muongozaji katika njia yako. Mafanikio unayotaka yanaanzia kwenye akili yako. Unapaswa kuwa tayari kubadilika kimwili na kiroho pia. 

Ni mengi unahitaji kufanya, wakati ndio huu kuyafanya. Hakuna wa kukuzuia kuyafanya. Ni wewe tu kukubali kubadilika na mabadiliko ya kweli unayotakiwa kuyapata yaanzie akilini mwako. Namna unavyoishi kuwa mtu mwenye focus, weka lengo kutimiza malengo. 

Hiyo yote ukiifanikisha amini maisha yako yatabadilika. Usijali kuhusu muda. Wewe jali juhudi unazoweka kuendana na mabadiliko hayo. 

Kumbuka, Umri sio shida. Kipato chako, mahali unapoishi vyote hivyo havina shida. Ukitaka kubadili chochote anza na wewe. Usikimbilie kutoa lawama kwa watu. Huenda walichangia kuanguka kwako lakini hiyo haiwezi kukuzuia kupata unachotaka.Badilisha mawazo na akili yako na kufanya kile kilicho sahihi. Hakika utafanikiwa. 

Je, ni kitu gani kinakuzuia kuendana na mabadiliko? 

Bonga nasi hapa hapa 0767702659 
Imeandaliwa na Lackius Robert 

No comments:

Post a Comment