Monday, March 20, 2023
Ukifanya hiki utajitoa kwenye mazoea
Saturday, March 18, 2023
Usichoke, ndiyo maisha yetu
Friday, March 17, 2023
Nini kinafanya wakuchague?
Thursday, March 16, 2023
Nguvu ya jina la kwanza
Monday, March 13, 2023
Unaweza kushinda mchezo wowote
Saturday, March 11, 2023
Mabadiliko yanaanza na wewe
Wednesday, March 08, 2023
Ni kidogo lakini kinampa faraja
Tuesday, March 07, 2023
Hiki ndicho huvunja uaminifu
Monday, March 06, 2023
Uwezo wako wa ushawishi umefichwa huku
Sunday, March 05, 2023
Maono na uwezekano
Saturday, March 04, 2023
Hii ndiyo sababu inayofanya usahau ulichojifunza
Friday, March 03, 2023
Tushirikiane sisi ni wamoja
Nilipata hamasa zaidi niliposoma hadithi inayosema kuwa:
"Kwenye Shule moja kulikuwa na kundi la wanafunzi watukutu ambao walikuwa wakionea wanafunzi wenzao. Wanafunzi hao walikuwa wakikuta mwanafunzi mwingine wanamlazimisha achague wa kupigana naye na akikataa wanampiga wote.
Siku moja kundi hili walikutana na mwanafunzi mmoja aliyeonekana kuwa mnyonge sana. Wakamwambia achague wa kupigana naye. Yule mwanafunzi akachora mstari na kusema yule ambaye anajiona ndio mbabe kuliko wote avuke huu mstari. Yule ambaye ndio alikuwa mbabe alivuka mstari ule na alipofika upande wa pili yule mwanafunzi mnyonge alimwambia sasa tupo upande mmoja, tuungane kupambana na hao wengine. Yule mbabe akakubali wakaliamsha kuwapiga wengine".
Unaweza kuona ni usaliti lakini sio kweli huyu mnyonge alimwambia neno la msingi. Huenda mtoto mbabe hakuwahi kulisikia. Maisha yeke yote aliishi kupigana na kushindana. Lakini alipoambiwa "tupo upande mmoja, hivyo tuungane pamoja". Aliona kuna jambo la msingi.
Hata maisha yetu ndivyo yalivyo. Mnapokuwa upande mmoja mnapaswa kuwa wamoja. Kushirikiana, kushauriana na kushirikishana katika masuala mbalimbali ya maendeleo.Bila kusahau watu wote wanaokuzunguka. Hao mpo nao upande mmoja. Ni vema kusaidiana na kushirikishana.
Tatizo ni kwamba wengi wetu hatuelewi hii dhana ya umoja. Ndio maana tumekuwa tunashindana lakini hatufiki mbali.
Mfano. Kama wanandoa wangejua kwamba wapo upande mmoja, wa kutaka maisha yao wote kuwa bora basi matatizo mengi sana ya ndoa yasingekuwepo na ndoa zingedumu. Lakini baadhi ya familia, unakuta mme anashindana na mke wake. Wakati mwingine mke anamuibia mali mme wake. Inashangaza sana.
Mwajiri na mwajiriwa hawa wote wapo upande mmoja. Kila mmoja yupo kunufaisha kazi yao na maisha yao kwa ujumla. Lakini mambo ni tofauti huyu anamkwaza na kumkandamiza mwenzake mara anamuibia. Vitu vya kushangaza vinafanyika.
Nashangaa kwanini tunafikiri kwamba tuko pande tofauti na hivyo kuishia kushindana, mashindano ambayo hayamfaidishi hata mmoja wetu. Mke na mme kushindana, kuibiana. Mtu na mdogo wake kunyanyasana, kutesana na kuibiana. Inashangaza sana.
Wakati ndio huu. Tushirikiane sisi ni wamoja. Tuache ushindani. Baba na mama jenga familia bora. Mwajiri na mwajiriwa ikuze taasisi yenu kupitia umoja. Hakika mtafanikiwa.
Je, nini kinazuia maendeleo yako?
Bonga nasi 0767702659
Imeandaliwa na Lackius Robert
#33mwangaza2023