Friday, September 20, 2019

Faida za kuwa mjasriamali bora

 MORNING MOTIVATION DIARY

Faida za ujasriamali

Ndugu,
Leo ni  siku nyingine tena kwenye program yetu pendwa ya morning motivation diary yenye lengo kubwa la kuiboresha siku yako na kuifanya iwe mpya.Karibu tujifunze faida za kuwa mjasiriamali:

Kuongeza kipato,
Hii ndiyo dhana ambayo kila mmoja wetu anahihitaji.Unapokuwa mjasiriamali unakuwa na uwezo mkubwa wa kuongeza kipato chako na kukudhi baadhi ya mahitaji ambayo pengine mshahara ulikuwa auyatimizi.
Kila mmoja ana ndoto nyingi ambazo anataka kuzitimiza,Kama ulikuwa unajiuliza utawezaje kuzitimiza basi jibu mojawapo ni kuwa mjasriamali ambaye anajituma na kufanya kazi kwa bidii.

Nikukumbushe ndugu yangu mpendwa,ili kuweza kuongeza kipato chako lazima uwe mpambanaji ,mbunifu inabidi uwe  mjasriamali ambaye anaenda na wakati.Tofauti na hapo utachukua muda mrefu kutimiza ndoto zako kama bado  auna vyanzo imara vya kipato chako.Hali ambayo itaendelea kukunyima Uhuru wako kifedha,Kumbuka mjasriamali wa Leo ni tajiri wa kesho.

Kuwasaidia watu wengine,
Katika kitabu cha My philosophy of success chake Jim Rhom katika sura ya pili kwenye "Falsafa ya utendaji na uzalishaji " anasema ili kufanikisha utajiri na ukuu katika dunia hii inabidi utafute namna ya kuwasaidia watu wengine.Tumia ujuzi wako kuhakikisha watu wanapata msaada wako, hivyo                     hutaweza kufanikiwa katika maisha yako kama bado auwasaidii watu wengine.Hapa ndipo watu wengi hufa wakiwa masikini bila wao kujua,kwa sababu ya kushindwa kuwasaidia watu wengine katika nyanja / kazi mbali mbali.

Nikukumbushe ndugu yangu mpendwa unapokuwa kuwa mjasiriamali unakuwa na uwezo wa kuwaajiri watu,kuwapatia huduma bora na ukizingatia katika kanuni za biashara kwamba mteja siku zote ndiye bosi.Hivyo unapokuwa unatoa huduma bora kama mjasiriamali unakuwa unajihakikishia ukuu na utajiri unaunyemelea.Angalia wajasiriamali wakubwa jinsi wanavyowasaidia watu mbali mbali wenye uhitaji,na wanapowasaidia ndivyo kazi zao zinavyozidi kusonga mbele zaidi.Unachotoa ndicho unachopata ni sawa na unavuna ulichopanda,kupitia ujasriamali wako waoneshe wengine jinsi ya wao kufika pale hakika utakuwa katika nafasi kubwa ya kufanikiwa zaidi.

Kutatua matatizo na kutumia fursa,
Malengo makubwa ya watu kuingia kwenye ujasriamali ni kutoa huduma bora kwa watu , kwa kuwasaidia kuwapatia hudumabora.
Kama tunavyojua fursa nyingi zinatokana na matatizo tuliyonayo au mahitaji mbalimbali tunayoyahitaji katika maisha yetu ya kila siku.
Mfano kama kuna watu wana uhitaji wa maji katika jamii /mtaa uliopo ,kama mjasiriamali ukitengeneza mfumo wa kuwapatia watu maji tayali umetatua tatizo la maji na umetumia fursa hio.Hivyo unawapatia maji na wao wanakupatia Pesa,inakuwa ni win win situation.

Nikukumbushe ndugu yangu mpendwa mafanikio yoyote tunayoyata yanategea sana kwa jinsi gani tunatoa huduma zilizobora kwa watu wanaotuzunguka.Hasa hasa kwa kutatua matatizo mbalimbali yanowakumba.

"Ushindi upo mikononi mwako kwa kuwa umebarikiwa".

Kwa mawasiliano zaidi 0767702659
Lackius Robert karibu.

No comments:

Post a Comment