Wednesday, December 04, 2019

UCHAMBUZI WA KITABU CHA EAT THAT FROG


MORNING MOTIVATION DIARY 
PRESENT: UCHAMBUZI WA KITABU
JINA: EAT THAT FROG, 21  GREAT WAYS TO STOP  PROCRASTINATING AND  GET MORE DONE IN LESS TIME. KULA HUYO CHURA ,NJIA 21 ZA KUEPUKA UGHAIRISHAJI NA KUFANYA MENGI KWA MUDA MFUPI.
MWANDISHI: BRIAN TRACY.
UTANGULIZI:

Brian Trace ni mwalimu mwenye uzoefu sana katika eneo la mafanikio. Baadhi ya mambo mengi ambayo Brian anatushirikisha ni yale ambayo amekuwa akijifunza, kisha anayafanyia kazi yeye binafsi na ndipo anatushirikisha kupitia vitabu vyake. Katika kitabu hiki ametushirikisha namna ya kupambana na hali ya kuahirisha mambo uliyopanga kuyafanya.
Ukweli kuhusu Chura
Mark Twain aliwahi kusema jambo kubwa unalopaswa kufanya kila asubuhi ni kula chura moja kwa moja."Chura" wako ndiye kazi yako kubwa na muhimu zaidi, ndio iliyo na uwezekano wa kuchelewesha ikiwa hautafanya jambo fulani juu yake. Pia ni kazi moja ambayo inaweza kuwa na athari nzuri zaidi maisha yako yote.
Sheria ya kwanza ya kula chura ni, "Kama utatakiwa kula vyura wawili, kula mbaya kwanza aliyebaki mmalizie baadae " ,Hii ni njia nyingine ya kusema kwamba, ikiwa una kazi mbili muhimu mbele yako, anza na kazi kubwa, ngumu na muhimu zaidi kwanza. Jiridhishe mwenyewe kuanza mara moja na kisha kuendelea mpaka kazi imekamilika kabla ya kuendelea na kitu kingine.Fikiria hii kama "jaribio.", Kataa jaribu la kuanza na kazi rahisi .
Sheria ya pili ya kula chura ni, "Ikiwa itabidi kula chura moja kwa moja, hailipi kukaa na kuiangalia kwa muda mrefu sana. " Ufunguo wa kufikia viwango vya juu vya utendaji na tija ni kwako kukuza tabia ya maisha yako yote ya kushughulikia kazi yako kuu kwanza kitu kila asubuhi. Lazima uendeleze utaratibu wa "Kula yako chura "kabla ya kufanya kitu kingine chochote, na bila kuchukua muda mwingi kufikiria juu yake.
Ndugu karibu tuzichambue sura moja baada ya nyingine ni matumaini kuwa  utafurahia pamoja na kuchukua hatua baada ya kufika mwisho wa uchambuzi wa  kitabu hiki.


SURA YA KWANZA,
Panga ratiba
Napoleon Hill aliwahi kusema"Kuna sifa moja ambayo mtu anayependa  kushinda anapaswa kuwa nayo , nayo ni kuweka kusudi  na ujuzi wa kile kitu ambacho ana hamu ya kukifanikisha. ”
Kabla ya kuamua kumla "chura" wako ili uendelee na kazi, lazima uamue unataka kufikia wapi kwenye  maisha yako.
Watu wengi wanashindwa kuyafikia malengo yao kwa sababu wanakosa motisha ya kufanya kazi ,kwa sababu hawana mwongozo ulio imara katika kuyafikia malengo waliyoweka.Utafiti unaonesha kuwa asilimia 3 ya walioweka malengo ndio waliofanikisha na wengine asilimia 97 walishindwa kuyafanikisha. Kuna hatua saba kama unahitaji kufikia malengo yako inabidi uzifahamu na kuzizingatia :
Hatua ya 1.Amua unataka uwe nani ,kaa chini tafakari chagua eneo ambalo unaona linakufaa lifanyie kazi.Steven Covey aliwahi kusema’’ kabla hujaamza kupanda ngazi ya mafanikio hakikisha ,ngazi imenininginia katika sehemu sahihi ya jengo’’
Hatua ya 2.Andika shehemu,Chukua kipande cha karatasi andika malengo yako ,wakati unaandika hakikisha unaandika malengounayoweza kutimizika ,yanayoonekana na kueleweka maana kuwa na malengo yasiyoandikiwa kunakupoteza.
Hatua ya 3.weka ukomo wa malengo yako,Maamuzi au malengo yasiyo na ukomo yanakuwa hayana uharaka ,hivyo unapopanga malengo hakikisha yanakuwa na ukomo ili kuepusha kughairisha mara kwa mara.
Hatua ya 4.Andika vitu vyote ambavyo unahisi ukiwa navyo vinaweza kukusaidia kuyafikia malengo yako.
Hatua ya 5. Pangilia vizuri mahitaji yako,weka vipaumbele/ pangilia vitu vya msingi sana unavyohitji ikifatiwa na vitu vingine amabvyo sio vya msingi sana.
Hatua ya 6. Chukua hatua,Fanya chochote, Mpango wa wastani uliotekelezwa kwa nguvu ni bora zaidi kuliko mpango wa kipaji ambao hakuna kitu kinafanyika .
Hatua ya 7.Amua  kufanya jambo moja kila siku lililo kwenye lengo lako,jitahidi kuzidi kujifunza zaidi na zaidi.

KUNA NGUVU KUBWA YA KUANDIKA MALENGO
Malengo ya maandishi yaliyo wazi yana athari nzuri kwa mawazo yako maana yanakuhamasisha na kukuchochea kuchukua hatua. Malengo ni mafuta katika tanuru ya mafanikio. Fikiria juu ya malengo yako na kuyapitia kila siku,Kila asubuhi baada ya kuamka, chukua hatua juu ya kazi muhimu zaidi unayoweza kukamilisha kufikia lengo lako muhimu zaidi kwa sasa.
SWALI:Je ni malengo yapi uliyojiwekea ili kufikia ndoto yako?.

Uchambuzi umefanywa na Lackius Robert kwa mawasiliano zaii 0767702659au maarifarobert@gmail.com

karibu  utatumiwa kwa njia ya PDF kupia whatsup,email,au tegegram.

No comments:

Post a Comment