Wednesday, December 18, 2019

MBINU ZA MAFANIKIO NA LACKIUS ROBERT


UCHAMBUZI WA KUHUSU MAISHA NA MAFANIKIO NA  LACKIUS ROBERT
Zingatia haya machache yafuatayo

 TABIA YA KUBAGUA KAZI;
Hakuna binadamu aliyeumbwa kufanya kazi fulani na mwingine afanye kazi ile sote tunafanya kazi kuendana na maisha yetu yalivo.utfiti unaonesha kuwa asilimia 80% ya kushindwa kufikika kwa malengo kunachangiwa na sisi  mwenyewe katika fikra zetu yaani inner feeling halafu asilimia 20% ni Sababu za nje,matumaini yangu makubwa kwamba wengi wetu tunazitambua changamoto zinazotukabili kwa ambao tupo kwenye masomo tunatambua kwamba changamoto kama vile  ajira ipo tumeisikia hata wengi wetu  bado hatujaingia kwenye elimu ya juu na cha kushangaza ni kwamba baadhi yetu pesa tunazopewa  na wazazi wengine wnapewa na bodi lakini tunazitumia katika matumizi ambayo wakati mwingine yasiyo sahihi simanishi kwa wote ila kama unazitumia katika matumizi ambayo sio sahihi inakuhusu na tutambaua mlima ulio mbele yetu kwenda nyumabani kulima hautaki wakati pesa unazipata umazitumia vibaya je nani wa kulamiwa mzazi wako serekali au nafisi yako.nayaongea hayo maana nimewatazama vijana wengi wakiangaika baada ya kuhitimu masomo yao,huku wakilaumu sana.

Pia vijana wenzangu baada ya kuhitimu masomo kubagua kazi kunakuwepo wapo wengine wanaona kazi kama vile kuuza maji ,kupakia mizigo ni kazi ambazo anaona hazimfai kabisa tunashindwa kutambua kwamba hio pesa yenyewe tunayoitafuta haijawahi kumbagua mtu yeyote ndio maana utajiri auna ubaguzi utakuta vijana wengine miaka ishirini ana pesa za kutosha mzee mwenye miaka sitini au hamsini ana pesa za kubabaisha ,wzazee wengine wanapesa za kuosha wengine wamesoma wengine hata chekechekea hawajaenda lakini pesa anazo kwa hio vijana wenzangu swala la kubagua linatufanya tunabaki kuhangaika tu mijini na vijijini.Kinachoshangaza ni kwamba unamkuta kijana mwenzangu hana hata mia lakini ukimwambia njoo basi tukapige kibarua hata kusomba tofali kwa siku elfu saba au elfu kumi anakwambia hizo kazi sio za kwetu wapo wenye uwezo kwa kuzifanya ,na je! pesa na yenyewe ingesema mi nataka nishikwe na huyu Yule hafai ingekuwaje au kama ingewachagua wasomi tu,au ambao hawajasoma duniani tungeishi je?.

Vijana wenzangu ambao hatupo kwenye masomo ni mengi sana tunayaona pamoja na kuyasikia redio mbali mbali zinatangaza viongozi mbali mbali wanasema kuhusu namna gani vijana tuwe na maisha mazuri.Mimi nafurahi sana ninapowakuta vijana wanajishughulisha na shughuli kama vile biashara ndogo ndogo siku moja nilikuwa Ubungo nikakutana na kijana mmoja anabeba mizigo kwenye mkokoteni na kuzipereka sehemu tofauti kutegemea na wasafiri wanapoelekea nikabaatika kuzungumza nae kwa kina akanieleza jingi gani anavyopenda kazi yake licha ya kwamba pesa anayopata sio nyingi lakini mahitaji ya familia anayapata pia na kulipa kodi ya nyumba..

Changamoto yetu vijana wengi tunadharau kazi hasa hasa zile za kutumia nguvu nyingi lakini tukumbuke imeandikwa kila mtu atakula kwa jasho lake ,mbuzi anakula kulingana na urefu wa kamba yake ila tunashindwa kufanya mfano mdogo wa kuku,nafukili wengi tunamjua jinsi gani anavyotafuta chakula chake kwa kuparua parua huku asipopata wadudu anageukia pale pale upande wa pili na kupata wadudu na kuwala .Vijana tuchotaka kuona ni kupata kazi nyepesi nyepesi kwa hali hio hatutafka mbali tuutume ujana wetu kufanya kazi nzito juani wakati  huo tukitegema kuvuna mazao tukiwa kivulini Walen Buffet anasema’ kivuli cha mti uliokalia leo kuna mtu aliupanda’kwa hio tupande mbegu bora kwa ustawi wa maisha yetu. Kila mtu anaouwezo mkubwa wa kufanya kazi yoyote endapo akilegeza mwili na kururusu moyo kuwa na  amani kwa kila kazi iliyoko mbele yetu. .

ILE HARI YA TAMAA;
Hali ya kutamani kitu fualani haiepukiki kwa maisha ya mwanadamu yeyote maana kutoka na kutamani ndiko tuapata ushindani pengine mafaikio pia wapo wanaotamani wazaliwe kama wachezaji wakubwa kama hapa Tanzania Mbwana Samatta kina Msuva na wengineo,wasanii wakubwa kama Diamond ,Lady Jay Dee ,waamashishaji maarufu kama Eric Shigongo,Nanauka Antony Luvanda na wengineo wengi tamaa ya namna hio kama tukitamani na kuongeza juhudi inakuwa ni nzuri .Kiuharisia kila mwanadamu anapaswa kutamani  tama mbele mauti nyuma maana kutokana na kutamani ndipo tunapata namna ya kusogeza maisha yetu mbele tama ipo katika Nyanja tofauti maana kila mmoja wetu  ana namna anavyotamani. 

Tamaa ya moyo, yaani tama hii Kwetu vijana imekuwa ni tamaa ambayo wakati mwingine hutususumbua na kuharibu mipango yetu ya maisha 20% katika wimbo wa’’ tama mbaya’’ anasema moyo sifa yake kutamani tama ya moyo inaweza kukuweka matatani. Mara nyingi tumekuwa tunatamani mambo makubwa kuliko uwezo wetu kama vile nyumba magari  nyingi wakati hatujaweka njia za kupata vitu hivyo na tamaa hiyo mara nyingi inapelekea kuhahirisha baadhi ya vitu tunavyokuwa tumeweka tumeona vijana wawili waliokuwa na mpango wa kujenga nyumba na mmoja wao akatamani ashobokewe na mabinti hadi akaamua kununua pikipiki ambayo hakudumu nayo muda mrefu na tama yake ilimponza.

Pia kuona kitu chochote kizuri moyo unakitamani kwetu vijana unamwona binti au mvulana mzuri moyo unamtani hadi akili nzima kichwani ivnavurugika unatamani kupata japo hata dakika kadhaa za kuzungumza nae ,uwepo pia wa mitandao ya kijamii umechangia sana vijana wengi kutamani sana maana kuna wengine wanapost picha zinazoonesha nguo za ndani ,aina mbalimbali za mitindo mara nywele,nguo n.k na sisi vijana tukiona wanapata comments na likes nyingi tunapata shauku ata kubadilisha miili yet undo wengine tunaona wanajichubua wananyoa mitindo tofati ya nywele na vijana wa kuime kutoboa masikio lengo ni kutaamani kuwa kama wale anaowaona lakini tutambue vijana  kusimama imara na kutunza miili yetu ni jambo ambalo linaleta heshima hata kwa jamii inayotuzunguka.

Tamaa ya pesa,jambo lisilo napingamizi kwamba kila mmoja wetu anataka awe na pesa za kutosha ili kujikimu kimaisha tama ya pesa hauwezi kuikwepa hata siku moja wengi tunaishia tu kutamani lakini hatuweki mipango madhubuti ya kupata pesa hizo inafika hatua wengi wetu wanaingia kwenye wizi,unyanganyi kwa watu wanoonekana wanapesa ,mali lengo ni kutaka kuwafanya hao vijana waingie katika ulimwengu wa matajiri.

Kuwa UNSTOPPABLE maana yake usitishiwe au kuyumbishwa na vitu vinavyoonekana havina tija kwa maisha yako ya kila siku,vijana tunyanyuke na kufanya kazi kwa bidii pes ipo ukiitafuta utaipata lakini kuendelea kulalamika pesa hakuna vyuma vimekaza hakutatusaidia kumbuka wanasema hata safari ya maili elfu moja huanza na hatua moja Yule tajiri tunayemuona anapesa za kutosha naye alianza na shilingi 100 na kuendelea je mimi na wewe tunataka tuanzie shilingi ngapi ?.

Jambo la muhimu kuzuia tama ya pesa kutusumbua tuweke ratiba maalumu ya kuwa tunatunza akiba kila baada ya kupata kiasi fuani cha pesa haijarishi tumetunza kiasi gani baada ya muda alienza na mia moja tutakuwa katika harakati za kumfikia .Natambua changamoto zipo kila siku na hazitaisha lakini najiuliza kama baadhi ya vijana wenzetu wamefaulu kuzishinda changamoto hizo wakawa unstoppable kwa nini mimi na wewe? Je! Wao wana miguu,macho na mikono  zaidi ya mbili? .

Tufanye maamuzi sasa wakati ndio huu, katika kutamani kupata pesa Elieshi Lema katika kitabu cha ‘’In the Belly of Dar es salaam ‘’ amejaribu kuonesha baadhi ya vijana wanaotamani kuja mjini wakifikilia kuna maisha mepesi na kukimbia maisha yao ya kijiji baada ya kufika mjini wanakuta ni tofauti kabisa na matarajio waloyawaza pindi wapo nyumbani baada ya kuona maisha yamekuwa magumu huanza kujiingiza katika matendo mabaya ikiweo kufanya ukahaba wizi n.k.

Tamaa hii mara nyingi inachochewa sana na makundi ya marafiki tunaokuwa nao nimesoma stori kadhaa za madada wenye kutamamani pesa za haraka mpaka wakajiingiza kwenye biashara ya kuuza mwili,vijana wengi wa kiume kuishia kucheza kamali lengo ni kutaka kuwa na pesa alizonzo Fulani katika kundi lao na hali hii ya tamaa humfanya mambo yasiyo na tija kubwa kwa maisha ya badae mfano madwa ya kulevya, mtu anakosa amani anafanya kazi kufa na kupona mpaka apate kama cha mwenzake badala ya hizo nguvu kuziweka katika maendeleo ambayo yatanufaisha familia yake na taifa kwa ujumla.

Mawasiliano zaidi 0767702659 Lackius Robert karibu sana. Ili kuendelea kupata chambuzi mbali za vitabu bonyeza link hii ili uendelee kupata ucambuzi wa vitabu kwa lugha ya kiswahili.
htthttps://t.me/SOMAONLINETELEGRAM




No comments:

Post a Comment