MORNING MOTIVATION
DIARY
PRESENT: UCHAMBUZI WA
KITABU
JINA: HOW SUCCESSFUL
PEOPLE THINK: Change your thinking,change your life
JINSI WATU WALIOFANIKIWA
HUFIKIRIA: Badilisha fikra zako, Badilisha maisha yako.
MWANDISHI : JOHN C.MAXWELL
UTANGULIZI
Wafikiriaji wazuri daima wanaangalia mahitaji,Wanatambua kazi
zao za kila siku na kila wakati ni watu wanaojua kwanini wao ni mabosi.Mara
zote hutatua shida zinazojitokeza katika sehemu wanazoziongoza iwe ni kwenye
kampuni au la kamwe hawapungukiwi na maini jinsi kuendesha uongozi wao,wanakuwa
na fikiri za mbali kuhusu kuwa na kesho ambayo ni bora.
Mwandishi John Maxwell anasema ,Nimejifunza zaidi ya
miaka arobaini na kugundua kuwa
kinachowatofautisha waliofanikiwa na wasiofanikiwa ni namna wanavyofikiri,waliofanikiwa
mara zote wanajua umuhumu wa kujifunza zaidi na uzidi kujifunza ukilinganisha
na watu wasio na mafanikio.
Kwanini unapaswa
kubadili fikra zako?
Japokuwa kubadili fikra zako sio rahisi lakini ukiamua
unazweza lakini unapswa ujue kwamba kubadili fikra hakuji automatiki lazima kuwe
na kichocheo ,hivyo kubadili fikra zako
kunakusaidia kutatua matatizo mbalimbali na kukutengengenezea fursa.Pia
unapelekea kuruhusu hisia zako kufanya kazi vizuri maana mfumo uwezo wetu wa
kufanya jambo lolote unaanzia katika fikra zetu ndipo matendo yanafatia.Ufikiriaji
mzuri unasaidia sana mtu kuyafikia malengo aliyoyaweka katika kazi zake ikiwemo
wale anaowaongoza.
Ilii uweze kuboresha zaidi ufikiriaji wako
Tafuta sehemu tulivu ambayo haina mizunguko ya watu ukae utulie
na uanze kutafakari kuhusu yale unayoyatamani kuyafanya baada ya kuyafikiria
vizuri na kuyaweka katika mipangilio mizuri hatua kubwa inayofuata ni kuyaweka
katika matendo.Jambo la kuzigatia ni kuwa unafanya hivyo mara nyingi ili kuweza
kuuzoesha ubongo wako ufanye kazi zaidi na zaidi mafanikio yako yanaongozwa na
fikra zako.
Ndugu karibu tuzichambue sura moja baada ya nyingine ni matumaini kuwa utafurahia pamoja na kuchukua hatua baada ya
kufika mwisho wa uchambuzi wa kitabu
hiki.
SURA YA KWANZA
Tengeneza picha kubwa ya kufikiria
David SCHWARTZ aliwahi kusema "Pale
ambapo mafanikio yanahusika, watu hawapimwi kwa nchi, pesa walizonazo au digrii
za chuo kikuu, au asili ya familia zao bali hupimwa kwa ukubwa wa mawazo na yao.
"
Unapokuwa umefikiri katika mapana ya picha kubwa ni njia
ambayo itakupa ufanisi wa fikra zako. Sifa kubwa waliyonayo watu wanaofikiri
kwa mapana ya picha kubwa ni kwamba daima huwa hawaridhiki na hali
inayowakabili muda wote bali wanakuwa macho kwa ajili ya fursa mpya. Watu hawa
wanajifunza kila mara kutoka kwa watu wengine na hivyo wanafanya kazi kwa bidii
na ubunifu katika shughuli zao kila siku. Watu hawa wanatambua nguvu kubwa
iliyopo kwenye usikivu kutoka kwa wengine kuliko kuwa wazungumzaji wakubwa.
Pia, watu hawa muda wote wanatazama mbali malengo yao makubwa ni kutafuta fursa
mpya ili wazifanyie kazi.
Kwa nini utengeneze picha kubwa ya kufikiria?
·
Kufikiria
mapana yenye picha Kubwa inakusaidia kuongoza,Kama kiongozi unapokuwa na picha
kubwa katika ufikiriaji wako unakuwa na maono makubwa kabla ya wengine
kuyaona,unakuwa unawaza ya kesho kabla yao,unakuwa na mitazamo ya kule
mnakoenda tofauti na wao waliyonayo.Ikiwa ni kujenga barabara, kupanga safari za
kikazi katika uongozi, mawazo ya picha kubwa hukuruhusu kufurahia mafanikio
zaidi. Watu ambao wanaangalia kila wakati picha nzima wana nafasi nzuri ya
kufanikiwa kwa juhudi yoyote.
·
Kufikiria
picha katika ukubwa Kunakupeleka kwenye mahali ulipolenga,Ili kufanya vitu
vizuri, unahitaji kufikiria jambo katika upana wake ikiwemo kulielewa na
kulifanyia kazi pasipo kusuburia.
·
Kufikiria
jambo kwa upana kunakusaidia kuona
wengine wanapoona ,Moja kati ya ujuzi ambao mtu yeyote anahitaji kuwa nao ni
uwezo wa kuona wengine wanapoona ,kwa kufanya hivyo hujikuta anawahudumia
wateja wake vizuri tena kwa kuwaridhisha lakini hali hii inaambatana na
ufikiriaji mzuri unaoendana na kuwa
unatafakari mambo katika ukubwa.
·
Kufikiri
jambo kwa upana kunasaidia kuboresha ushirikiano kwa kufanya kazi kwa pamoja na
kuboresha mahusiano ikiwemo kusaidia na hii upendeza watu wanaofikiria mambo
kwa upana zaidi wanapokutana.
Hivyo ili kuweza
kuboresha uwezo wako wa kufikiri jambo kwa upana zaidi unatakiwa kujifunza
kutoka katika kila uzoefu unaopitia au pale unapokuwa unafanya kazi na wengine
mkabadirishana mawazo ya hapa na pale.Unapokuwa na wazo sahihi, unatakiwa uwashirikishe watu sahihi
kwa ajili ya wazo husika, wazo pia lazima lishirikishwe katika mazingira
sahihi, muda pia unatakiwa uwe sahihi.
SWALI : Je nafikiri zaidi yangu,ulimwengu wangu ili niweze kushughulikia maoni kwa
mtazamo kamili?.Karibu upate sura ya pili mpaka mwisho wa kitabu hiki
No comments:
Post a Comment