MORNING MOTIVATION DIARY
PRESENT: UCHAMBUZI WA KITABU
JINA: OVER COMING PROCRASTINATION,
ISHINDE TABIA YA KUGHAIRISHA MAMBO
MWANDISHI : JOEL NANAUKA.
UTANGULIZI:
Moja ya sababu kubwa ambayo inawafanya wengi kushindwa kutimiza
malengo yao kwa wakati ni kughairisha mambo.Wengi wetu tunaseam ngoja niache
kidogo ntamalizia baadae lakini baadae inapofika tunajikuta tayali tuna mambo
mengine ya kufanya ilo tunalisahau.
Mwandishi Nanauka anaanza kwa kuuliza
“Unakumbuka wakati watu wametangaziwa
kujisajili kwaajili ya kupiga kura? Unakumbuka watu walivyotangaziwa kuhusu
usajili wa vitambulisho vya utaifa? Ni siku gani watu walijaa zaidi? Bila
shaka, utakumbuka ni siku ya mwisho hata kama waliliona tangazo. Kuna watu kila
siku wanatuma maombi ya kazi siku ya mwisho hata kama waliliona tangazo hilo
miezi miwili kabla. Kuna watu kila wakati watatuma ripoti yao siku ya mwisho,
kuna watu kila wakati kazi waliyopewa kufanya wataiwasilisha dakika za
mwisho”.Bila kujua madhara mkubwa yanayotokea baadae ,wengi wao hujikuta katika
hali ya kuwa na stress(msongo wa mawazo) maana ata kazi wanapozifanya zinakuwa
hazina ubora mzuri na hufanywa kwa kiwango cha chini kabisa na hali hii utokana
na tabia ya kughairisha.Anasema alimia 95 ya wazee walipoojiwa walisema
tunajuta kwa kughairisha mambo mengi
katika maisha yetu ambayo tungeyafanya basi tungekuwa mbali zaidi.Huo ndio
ukweli watu wengi wameghairisha mambo mengi tena ya msingi na kujikuta hawawezi
kuyafanya tena.
Ndugu karibu tuzichambue sura moja
baada ya nyingine ni matumaini kuwa utafurahia pamoja na kuchukua hatua baada ya
kufika mwisho wa uchambuzi wa kitabu
hiki.
SURA YA KWANZA
Kwa nini watu wanaghairisha
mambo?,utafiti wa kisayansi kuhusu kughairisha mambo.
Utafiti uliofanywa na William James ambaye ni mtaalamu wa
saikolojia uliochapishwa katika jarida la sayansi ya saikolojia mwaka 1997 akishirikiana na Dianne Tice ambao
uliwahusisha wanafunzi kutoka chuo kikuu cha Western Reserve uligundua kwamba wanafunzi
waliokuwa wanaghairisha walikuwa na msongo wa mawazo kuliko wanafunzi wasioghairisha
hali hii ilikuwa inatokea hasa hasa katika ukusanyaji wa kazi(assignment) kwa
mwalimu husika.Wakati wanafanya hivyo wanakuwa hawaoni Kama ni tatizo lakini
baadae linakuja kuwa tatizo ,na mwishowe walijikuta hata kazi zao hazina ubora
ukilinganisha na wanafunzi amabo walikuwa hawaghairishi mambo.
Mwandishi amebainisha taswira halisi katika maeneo ya
kazi. Anasema wapo wafanyakazi ambao hawapendi kutekeleza kazi zao kwa wakati
badala yake wanasubiri hadi dakika za mwisho ndipo waanze kuhaha huko na huko.
Kimsingi tabia hizi zinazozungumzwa zinawagusa watu wa kila kaliba. Haijalishi
umri wala nasaba au jinsia, Unaweza ukachukua daftari lako kuandika, ama ripoti
yako ama hata kusoma kitabu, ukaamua kuwa unafanya unachotaka kwa nusu saa bila
kuyumbishwa na kitu chochote, ghafla baada ya dakika 10 unajikuta nunashika
simu na unasema ngoja niangalie meseji, kuja kushtuka unajikuta umeshatumia
takribani nusu saa kuperuzi mitandao na hamu ya kuendelea na kazi uliyokuwa
unaifanya inapotea kabisa. Ama wakati mwingine unasema ngoja niangalie TV
kidogo kisha nitalala ama nitasoma kidogo, kuja kugundua unakuwa imeshafika saa
7 usiku na umeshindwa kuondoka kwenye TV yako.
Katika muktadha huo mwandishi anakumbusha kuwa wapo watu
wanaoishi kwa kuahirisha. Wengine ambao hadi wakumbushwe ndipo hutekeleza jambo
fulani. Wapo watu ambao hawezi kujikita kwenye eneo husika.
Mwandishi anatumia utafiti wa Profesa Joseph Ferrari
ambaye aligundua kuwa takribani asilimia 20 ya watu duniani ni waahirishaji
wakubwa wa mambo yao,ambapo ufafanuzi wake umejikita katika mifumo miwili
iliyopo kwenye ubongo kwa jinsi inavyoshindana.
Kuna mfumo unaitwa Limbic
system huu una sehemu ambayo ndiyo unahusika na wewe kujisikia raha unapofanya
jambo Fulani,mfano unapokula chakula kizuri,unapofanya tendo la ndoa na
mengineyo.
Mfumo wa Prefrontal
Cortex huu ni mfumo upo nyuma ya kipaji chako cha uso kazi yake kubwa ni
kukuongoza katika kufanuya maamuzi mbali mbali.Huu ndio mfumo unaokusaidia
kujua kipi kizuri na kipi kibaya kupitia tathimini hiyo unaweza kufanya
tathimini ya kila kitendo amabacho unakifanya na kupima madhara yake.Hiyo ndiyo vita inayoendelea katika ubongo
wako katika mambo mbalimbali unayotaka kufanya.
Unaporuhusu mfumo wa limbic kuwa na nguvu kuliko
prefrontal cortex ambao ndio una uwezo wa kufanya maamuzi basi utajikuta
unakosa hamasa na kuwa mgairishaji mzuri ambapo madhara yake ni kukosa nidhamu
ya muda, kuhisi una mambo mengi yasiyokwisha sababu ya kutotekeleza kwa wakati
na kulimbikiza majukumu ,utakosa hamasa ya kufanya jambo pia utakosa kuweka vipaumbele.
karibu ujipatie sura ya pili na kuendelea .....
No comments:
Post a Comment