Saturday, April 25, 2020

UCHAMBUZI WA KITABU CHA KITABU CHA THINK ANDA GROW RICH NAPOLEON HILL

KARIBU KATIKA SEHEMU INAYOFUATA YA UCHAMBUZI WA KITABU CHA THINK AND GROW RICH  NAPOLEON HILL.


4.Kanuni ya nne kuelekea utajiri ni kupata MAARIFA MAALUMU
Kuna aina mbili za maarifa moja ni ujuzi wa jumla na mwingine ujuzi maalumu.Ujuzi wa jumla pasipo kujali ni mkubwa kiasi gani au ni mwingi kiasi gani una matumizi kidogo sana katika kujipatia pesa.Ujuzi aupati pesa kama haujapangiliwa  na kuongozwa kwa akili kupitia mipango inayotekeleka ya kivitendo kuelekea kwenye lengo lililokuwa dhahiri la kujipatia pesa unayoitaka.Hapa watu wengi waga  wanachanganya na kusemea ujuzi ni nguvu ya kufanya upate unachotaka ,hii haiwezi kutimizika endapo auna mipango mizuri inayotekelezeka.

Mfano ukiangali katika vitengo mbalimbali vyuoni vimejaa watu wenye elimu kubwa,wastarabu na wabobezi lakini linapokuja swala la ujuzi bado hawajabobea katika kuyapanga na kuyatumia maarifa zaidi na kuwafanya wawe matajiri.Ukija kuangalia mtu aliyeelimika siyo lazima awe ni Yule mwenye ujuzi mwingi wa jumla au maalumu.Bali ni wale walioelimika na wamejenga vitivo vya vya akili zao kusudi ziweze kupokea kitu chochote wanachotaka mfano Henry Ford hakuwa na elimu kubwa lakini alikuwa ana uwezo mkubwa wa kuthubutu kufanya jambo pasipo kurudi nyuma tofauti na wengine wanavyoishia njiani.Mtu yeyote aliyeelimika  ni Yule ambaye anaweza kupata maarifa anayoyahitaji,najinsi ya kuyapangilia hayo maarifa katika mipango dhahiri ya kivitendo kupitia sehemu mbali mbali inaweza kuwa kundi lake la kushauriana n.k. 
 
Kabla hujaweza kuwa na uhakika wa uwezo wako wa kubadilisha shauku kuwa katika kiwango chake cha fedha kinacholingana nayo,unahitaji ujuzi maalumu wa huduma,bidhaa au utaalamu unaokusudia kuutoakwa ajili ya kupata utajiri.Pengine unaweza kuhitaji ujuzi maalumu zaidi kuliko vile ulivyokuwa nauwezo au mwelekeo wa kuupata na kama hii itakuwa kweli,unaweza ukauziba udhaifu wako kupitia kundi lako la kushauriana.Mfano Endrew Carnegie hakuwa  anajua kitu kuhusu biashara ya chuma cha pua na hakujisumbua bali ujuzi aliouhitaji aliupata kutoka kwa mmoja kati ya kundi lake la kushauriana.Ukihitaji kuwa tajiri inabidi uongeze jitihada kupitia ujuzi maalumu uliopangiliwa vizuri sana.

Amua juu ya aina ya aina ya ujuzi unaohitaji kuwa nao lengo unalofanyia kazi ili kulifikia na hapa inabidi ujiulize kuhusu taarifa na vyanzo sahihi vya maarifa unayopata;
(i)Uzoefu na elimu ya mtu mwenyewe
(ii)Uzoefu na elimu vinavyopatikana kupitia ushirikiano na watu wengine
(iii)Makataba za umma au kupitia  vitabu na majarida mbalimbali
(iv) Kozi maalumu za mafunzo kama kupiti mafunzo ya madarasa ya jioni na zaidi mfumo wa njia za posta.Hivyo ujuzi maalumu,pamoja na ubunifu  ni viungo bora vya kukufanya wewe kufanikiwa katika kila kitu aunachokifanya.

5.Kanuni ya tano kuelekea utajiri ni kuwa na UBUNIFU
Ubunifu maana yake ni karama ambayo mipango yote inayopangwa na mtu hutengenezwa.Msukukumo shauku hupewa umbo au vitendo kupitia msada wa kitengo cha ubunifu wa akili.
Kuna msemo wa kuwa ,tunaweza kutengeneza  chochote kile ambacho tunakifikiria.Katika zama zote za ustarabu,hizi ndiyo zama zinazofaa zaidi kwa ajili ya ukuzaji na ubunifu kwa sababu ndiyo zama za mabadiliko ya haraka sana.Karibia kila mahali tunakutana na vichocheo vinavyotufanya tuweze kubuni vitu mbalimbali.

Kwa sasa wapo wabunifu mbalimbali mbao wamefanya mambo makubwa ya kuishangaza dunia pia na kuisaidia dunia,hsahasa katika kutatua baadhi ya matatizo mfano waliobuni ndege,meri ,Gaari,vifaa vya mawasiliano kama simu tarakirishi na vitu vnginevyo vingi.Ndugu yangu mpendwa unawezaa ukabuni kitu kwa sasa na kisakusaidia wewe lkutataua baadhi ya matatizo yanayoikumba jamii na kukusaidia wewe mwenyewe.

Mwandishi anaonesha aina mbili za ubunifu:
1.Ubunifu sanisi,Hapa mtu anaweza akapanga fikra za zamani,mawazo au mchanganyiko mpya.Kitivo hiki akiumbi kitu chochote, bali hufanya tu kazi na vitu kama uzoefu,elimu na ushuhuda ambavyo kinalishwa.Kinatumika sana an wagunduzi,ukiacha watu wenye akili nyingi sana ambao hutumia ubunifu wanaposhindwa kutatua tatizo kupitia ubunifu sanisi.

2.Ubunifu wa kujenga,Kupitia kitivo cha ubunifu wa kujenga,akili ya mwanadamu  inayo mawasilianao ya moja kwa moja na nguvu ya uumbaji,hiki ni kitivo ambacho hutumia hisia na ufunuo unaopokelewa yaani hapa mtu anaweza kuwasiliana na akili za watu wengine mfano( mzuri angalia mafundisho ya dini yalivyo unaweza kuelewe ufunuoni nini).Kitivo hiki huwa makini kwa sababau kinahusiana na uwezo wa kutuia hisi za wngine na mara nyingi hufanya kazi chenyewe lakini katika umakini mkubwa sana.

Hivyo kadili kitivo chako cha ubunifu kinavyotumika ndivyo kinavyozoidi kuwa bora na kisivyotumika ndivyo kinavyokuwa dhaifu.Kumbuka kuibadili shauku ya kuwa na pesa siyo jambo linalofanyika siku moja au kwa akauli moja inabidi lifanyike mara nyingi   ili akili na viungo vyako vya mwili vizoee.Viongozi wakubwa wa biashara makampuni,viwanda fedha wasanii waandishi wakubwa wameweza kufanikiwa kwa sababu walikuza vitivo vyao vya ubunifu.Shauku ni wazo tu ,msukumo ni kama nyota ya mbali sana au wingu la muda mfupi sana,nikitu kisichoshikika ni kitu kisocho na thamanimpaka kigeuzwe kuwa kitu kinachoshikika.Hapa ubunifu sanisi ndio unaotumika mara nyingi zaidi katika mchakato huu wa kubadilisha msukumo wa shauku kuwa pesa.Unapaswa kuelekeza umakini wako katika kubdili ubunifu wako sanisi kuwa unaoshikikia maana unahitaji pesa an pesa ni kitu kinachoshukika.Una mipango mbalimbali pesa inabidi itumike uwezi kumwambia mtu ninamipango mbalimbali lakini pesa sina kwa sasa ntakulipa nikiipata ,hapo mtu hawezi kukuelewa. Kila kitu uanweza ukakifanya kwa sababu kimeshawahi kufanyika kabla.

Jiulize ningefanya kitu gani kama ningepewa dola milioni moja
Penye nia pana njia’ Nilisimuliwa na yule mpendwa mwalimu na mchungaji, Frank W. Gunsaulus, ambaye alianza kazi yake ya kuhubiri katika eneo la Stockyards la Kusini mwa Chicago.Wakati Dr. Gunsaulus alipokuwa chuoni, aligundua mapungufu mengi katika mfumo wetu wa elimu, mapungufu ambayo aliamini angeliweza kuyarekebisha ikiwa kama angelikuwa Mkuu wa Chuo. Shauku yake kubwa kabisa ilikuwa ni kuwa kiongozi mkuu wa chuo cha elimu ambacho vijana wadogo wa kiume na wa kike wangeweza kufundishwa “kujifunza kwa vitendo”.

Alifanya uamuzi wa kuanzisha chuo kipya ambacho angeweza kutekeleza wazo lake jipya pasipo kulemazwa na njia za jadi za utoaji elimu. Alihitaji Dolla Milioni moja ili kutekeleza mradi ! Ni wapi angelaza mikono yake kwa kiasi kikubwa hivyo cha pesa? Hilo lilikuwa ni swali lililotawala sehemu kubwa ya mawazo ya mhubiri huyu kijana aliyekuwa na malengo makubwa.
Lakini hakuweza kuonekana kupiga hatua yeyote.

Kila siku aliingia kitandani na lile wazo. Aliamka nalo asubuhi alitembea nalo kila mahali alipokwenda. Aliligeuza tena na tena katika akili yake mpaka likageuka kuwa shauku isiyotulizika. Dolla Millioni moja ni fedha nyingi. Alitambua ukweli huo lakini pia aligundua ukweli kwamba kikwazo pekee ni kile ambacho mtu hujiwekea katika akili yake mwenyewe
Alikuwa mwanafilosofia na pia mhubiri, Dr.Gunsaulus alitambua, kama wafanyavyo wale  wote wanaofanikiwa maishani kuwa, udhahiri wa lengo ndiyo kituo ambapo mtu ni lazima aanzie. Alitambua pia kwamba udhahiri wa lengo huchukua umbo, uhai na nguvu unaposaidiwa na Shauku kubwa kulibadilisha lengo hilo kuwa katika kitu kinacholingana nalo.Alifahamu ukweli wote huu mkubwa, lakini bado hakujua ni wapi au ni jinsi gani angeweza kuweka mikono yake kwenye dola milioni moja. Utaratibu wa asili ingeliweza kuwa ni kukata tamaa na kuacha, akisema , ‘Ah sawa, wazo langu ni zuri lakini siwezi kufanya nalo chochote kwa sababu kamwe siwezi kupata dolla millioni moja zinazohitajika’. Hivyo ndivyo hasa ambavyo watu wengi wangeliweza kusema, lakini sivyo Dr. Gunsaulus alivyosema.Alichosema yeye, na alichokifanya, ni muhimu kiasi kwamba sasa namtambulisha na kumuacha azungumze, mwenyewe.

Siku moja Jumamosi mchana nilikuwa chumbani kwangu nikifikiria njia na namna ya kupata fedha ili kutekeleza mipango yangu. Kwa karibu miaka niwili nilikuwa nikifikiria, lakini sikuwa nimefanya chochote zaidi ya kufikiria.
Muda ulikuwa umewadia wa kuchukua hatua !
Niliamua mara moja kwamba ningeweza kupata dolla milioni moja zilizohitajika, ndani ya wiki moja. Ki vipi? Sikujali kuhusiana na hilo. Jambo kubwa na la muhimu lilikuwa ni uamuzi wa kuzipata fedha ndani ya muda uliopangwa. Dakika niliyofikiria uamuzi huo, hisia ya ajabu ya kujiamini ilinijia kwa namna ambayo kamwe sikuwahi kuhisi hapo kabla. Kitu ndani yangu kilionekana kusema, “Kwanini hukufikia uamuzi huo muda mrefu? Pesa zilikuwa zikikusubiri muda wote !”
Mambo yalianza kutokea kwa haraka. Niliita magazeti na kutangaza kuwa ningeweza kutoa mahubiri(hotuba) asubuhi ya siku iliyofuata yanayohusu, “Ningefanya nini kama ningepata Dola million moja”.‘Nilikwenda kuifanyia kazi hotuba ile mara moja. Ni lazima nikueleze, ukweli haikuwa kazi ngumu kwasababu nilikuwa nikiiandaa hotuba hiyo kwa karibu miaka miwili. Roho yake ilikuwa sehemu yangu !muda kabla ya usiku wa manane nilikuwa nimemaliza kuandika hotuba. Niliingia kitandani na kulala na hisia za kujiamini kwani niliweza kuona mwenyewe kama tayari nilikuwa nazo dolla milioni moja.

Asubuhi iliyofuata niliamka mapema, nikaenda bafuni, nikasoma hotuba, kisha nikapiga magoti na kusali ili hotuba yangu iweze kusikika na mtu ambaye angeliweza kutoa pesa zilizohitajika.‘Wakati nikiwa nasali, tena nilijiwa na zile hisia za kujiamini, kwamba pesa zingeliweza kupatikana haraka. Kwa taharuki niliondoka bila kuchukua hotuba yangu, na sikugundua kosa hilo mpaka nilipokuwa kwenye mimbari yangu na karibu kuanza kuhutubia.

‘Muda ulishakwenda mno kurudi tena kuchukua karatasi, Baraka iliyojea akili yangu ilifikiria vyote ninavyohitaji niakavisema nilipomaliza mikakati ,wakati nimeketi mwanamme mmoj alikuja mbele akanishika mkono akaseam nimeipenda hotuba yako unaweza kupata kiasi hicho ukichokihitaji naitwa Philip Armour.Kesho asubhu alienda ofisini kwake akapewa hicho kiasi cha pesa akaanzisha taasisi ya teknolojia Armor.Dola milioni moja zilipatikana kutokan ana wazo liliotokana ana shauku aliyokuwa nayo muda mrefu,Ndani ya dakika 36 mpango wake ulikamilika na kufanikiwa kupatab kila alicho kihitaji.
Unaweza kupata chochote unachokihitaji kwa kutumia ubunifu wako.

6. Kanuni ya sita kuelekea utajiri ni KUWEKA MIPANGO MATHUBUTI
Umeshajifunza kuwa kila kitu kinachoumbwa na kumilikiwa ukianza na shauku.Shauku hiyo huchukua safari yake ya mwanzo pasipokuwa na kitu chochote mpaka kwenye kitu kinachoweza kushikika katika karakana ya ubunifu mahali ampapo mipango kwa ajili ya mabadiliko huandaliwa.
Katika sura ya pili ulielekezwa kuchukua hatua kama hizi  za kivitendo amabayo kupitia hizo mageuzi haya yanaweza kufanyika.Hapa uanelekezwa namna ya kutengeneza mipango kuwa vitendo:
1.Shirikiana wewe mwenyewe na kundi la watu wengi kadili utakavyohitaji kwa ajili y kutengeneza na kutekeleza mpango wako au mipango yako ya kujichumia fedha,ukitumia kanuni ya ‘’ushirika wa kushirikiana unaleta maendeleo’’.

2.Kabla ujaunda ushirika wako wa kushauriana amua faida zipi na manufaa unayoweza kutoa kwa mwanachama mmoja mmoja wa kundi lako kama malipo ushirikiano wao,hakuna mtu atakayefanya kazi milele pasipokuwa na malipo au kumtegemea mwingine afanye kazi pasipokuwa na malipo yanayofaa ingawaje malipo yale yanaweza yasiwe ya pesa moja kwa moja.
3.Panga kukutana ana wanachama awa kundi lako la kushauriana anagalau mara mbili kwa juma au zaidi kwa malengo makubwa ya kuwezesha uwezekano wakuchuma zaidi pesa.
4.Dumisha masikilizano kati yako na wengine amabao ni wana kikundi cha kushauriana,maana popote pasipo na kusikilizana amna  kitu chochote kinachoendelea,Katika hili zingatia kuyatenda majukumu yako kikamilifu pia kuangalia uezo na ubunifu wao.
Hakuna mtu yeyote mwenye uzoefu wa kutosha,elimu,uwezo wa asili wa kuhakikisha anajipatia utajiri pasipokuwa na ushirikianao na wengine.Mipango mingi inafanikiwa mkiwa katika kundi kubwa la kushauriana pamoja na kuchangiana mada mbalimbali ,maana kuna mipango utakayopanga .Hii itaangaliwana wengine ambao mko nao katika kikundi cha kushauriana.

Ukitengeneza mpango ukashindwa usiache anza upya na mara nyingi zaidi ili ifike hatua ufanikiwe.Mfano Thomas Edison alishindwa zaidi ya mara 1000 kabla hajafanikisha kuunda balbu ya umeme,katika hali hiyo alikutana na vikwazo vingi sana mpaka kufikia hatua ya kubwa ya kuiwasha balbu hiyo.Henry Ford alipata utajiri si kwa sababu alikuwa na akili nyingi bali alikubali kufuata mipango mathubuti mpaka akafanikiwa ,lakini wapo wengi wanaopewa elimu bora kuliko ya Ford lakini bado ni maskini kwa sababu hawana mipango mizuri.
Hakuna mfuasi wa falsafa hii anayeweza kwa makusudi kutegemea kupata utajiri pasipo kukutana na anguko fulani,Anguko linapokuja ni ishara kwamba mipango yako siyo mizuri tengeneza upya mipango yako vizuri usiachie njiani.’’Muachaji kamwe hashindi ,mshindi kamwe haachi’’.
Unapokuwa unachagua watu wa kushirikiana naoa jaribu kuangalia watu wanajari ,wasiopenda kuanguka anguka.wajasiri,amabo wanaweza kujizuia binafsi,matazamo ,uwezo wa kuamua wanaoweza kutengeneza mipango mathubuti hao ndio wanaoweza kukupatia mafanikio/utajiri.

7.Kanuni ya saba kuelekea utajiri ni MAAMUZI

Katika sura hii mwandishi anasema utafiti wa kweli uliofanyika kwa watu zaidi ya 25000 unaonesha wengi wao kitu kinachofanya wanashidwa kufanikiwa ni kushindwa kufanya maamuzi.Wengi wao wanashindwa kufanya maamuzi ya haraka na kuyaghairisha kitu kinachowaletea madhara baadae.
Kuna wakati tunaona fursa ila kutokana na kwamba adui mkubwa kughairisha ametuzingira hivyo tunajikuta tunaipoteza fursa ile.Mfano wa mtu ambaye alikuwa na uharaka katika kutoa maamuzi alikuwa ni Henry Ford amabaye alikuwa ni mkurugenzi wa magari ya “Ford”ambayo yaliamika kuwa na kasi sana.

Watu wengi hushindwa kupata mahitaji yao ya msingi hasa hasa ya kifedha kutokana na kusikiliza maoni ya watu na kuruhusu majungu kutoka kwa ndugu na majirani na kujikuta wanashindwa kufanya maamuzi mazuri wakiofia kuwapoteza.Ili kuweza kuwa na maamuzi mazuri badala ya kufungua mdomo na kuanza kuwaambia yaliyo yako ,Funga modomo fungua macho na masikio ukiufuata ushauri huu utakusaidia sana kuufikia utajiri.Simamia maamuzi yako ,simamia imani yako.Maamuzi ni baba wa IMANI na UJASIRI
Socrate aliona bora kunywa sumu kuliko kubadilisha imani yake na huu ulikuwa ni uamuzi wa busara kwa sababu mengi aliyoyafanya yameisaidia dunia hata na vizazi vinavyokuja.Jiulize je! Maamuzi yangu kuelekea utajiri ni yapi?.

8.Kanuni ya nane kuelekea utajiri ni  UVUMILIVU
Mwandishi anajaribu kuelezea kwa jinsi Uvumilivu ulivyo kitu cha msingi sana  ambacho msingi wake unaleta hamu nia katika ushindi.
Amejaribu kuonesha dalili za mtu mwenye uvumilivu na vitu anavyokuwa amepanga kama ifuatavyo;
(i)malengo ya vitu anavyotaka kuvipata kwa kipindi Fulani. (ii) Hamu ya kufanya kazi yake muda wote. (iii) Anayejitegemea. (iv) Mipango mizuri ya kazi zote anazotaka kuzifanya ili kuufikia utajiri. (v) Anatumia ujuzi  alionao katika kuyatatua magumu anayopitia. (vii)Ushirikiano. (viii) Yuko tayali kubadili tabia mpya lengo kuu ni kuufikia utajiri .
Pia mwandishi amejaribu kuonesha dalili za mtu anayekosa uvumilivu vitu anavyokuwa navyo au anavyoonesha;

(i) Kushindwa kuwa dhahiri kuwa na kitu anachokitaka hapa unamkuta mtu mara anataka kile,ajakaa sawa anataka kingine yeye muda wake wote ni kutaka vitu vingi pasipokuwa na msimamao wa kitu kikbwa kimoja anachotaka.(ii)Mtu wa kughairisha mambo bila kuwa na sababu yoyote. (iii)Anakosa hamu ya kupata maarifa mengine zaidi. (iv)Anakosa kuwa na maamuzi ya msingi mara kwa mara. (v) Tabia ya kuwategemea wengine badala ya kutengeneza njia za kutatua changamoto. (vii) Anakosa matumaini katika kile anachofanya (viii) Anapenda kulalamika kwa makosa madogo madogo yanayofanyika. (ix) Anakosa nia na ni mtu wa majuto muda wote .(xi) Anakosa mipango imara. (xii) Analalamikia umasikini badala ya kuwazia utajiri (xiii) Anapenda kupata badala ya kutoa .(xiv) Anatufa njia za mkato kuupata utajiri (xv) Anaofia sana kukosolewa .

9.Kanuni ya tisa kuelekea utajiri  NGUVU YA AKILI
Mastermind ni kuwa na timu ya watu mahali, ambayo kazi yake ni kukusaidia kufanikiwa na kutekeleza mipango yako. Katika hali hii unachagua watu wanaoendene na wewe kimawazo ili muweze kusaidiana. Hakuna mtu anayeweza kupata nguvu  kubwa ya mafanikio bila ya kuwa na nguvu ya akili yaani mastermind. Kusudi la mastermind ni kubadili maarifa kuwa nguvu, kwa kupanga mipango kuwa  dhahiri  kisha kutafsiri mipango hiyo katika matendo.Jiulize je !watu wangu ninaoungana nao kila siku ni wakina nani?, Majibu yako yafanyie kazi.

10. Kanuni ya kumi kuelekea utajiri SIRI YA USAMBAZAJI WA NGONO
Kitendo hiki huleta furaha kubwa miongoni wa wawili wafanyao kwa wakati sahihi maana huleta hali ya ujasiri, utashi, uvumilivu na uwezo wa ubunifu ambao haujulikani na watu wakati mwingine.Pia ameizungumzia siri ya usambazaji wa ngono katika makundi makubwa matatu;
(i) Utangulizi wa wanadamu
(ii) Utunzaji wa afya
(iii) Mabadiliko ya upatanishi kuwa fikra.
Japokuwa ngono ni nzuri lakini anasema inabidi ifanyike kwa wakati sahihi maana ikiendekeza inaweza kumpoteza mtu kufika katika safari yake ya mafanikio.

11.  Kanuni ya kumi na moja kuelekea utajiri AKILI YA CHINI YA UFAHAMU
Akili ya chini ya fahamu (sub conscious mind ) ni kiunga kinachounganisha kati ya akili laini ya mwanadamu na akili isiyo na mipaka. Akili ya chini ya ufahamu inaweza kutumika kama njia ya kupitisha tamaa zako kuwa sawa na za mwili au pesa.lakini, ukishindwa kupanda matamanio yako ndani yako hautapata matokeo mazuri.
Ili kupata udhibiti wa akili yako unapaswa kutumia faida hizi zifuatazo kuu za hisia zifuatazo: Tamaa, Imani, Upendo, Jinsia, Ushirikiano na Tumaini.
Unapaswa kupata ufahamu zaidi katika vitu hivi ili kuweza kuifikia safari yako ya utajiri Hofu, Wivu, chuki, kulipiza kisasi, Penzi, Ushirikina, Hasira.Tumia ufahamu wako vizuri kwa ajiri ya manufaa yako.

12. Kanuni ya kumi na mbili kuelekea utajiri  ni UBONGO
Mwandishi analinganisha ubongo kama kituo cha Utangazaji ,Kupokea na Kufikiria,Kila ubongo wa mwanadamu ni kituo cha utangazaji na kupokea kwa mtetemeko wa mawazo kutoka sehemu tofauti tofauti.Ubongo wetu na wanyama wengine hauna tofauti kubwa ila tumewashinda tu kwenye kufikiria na kuchukua hatua lakini wao wanaendeshwa kwa hisia tu.Hivyo kama mtu unayetaka kuwa na utajiri kifedha lazima kuruhusu ubongo wako kufikiria kisawa sawa na kuchukua hatua juu ya maisha yako.Kufikiria kunapaswa kuambatana na ubunifu mkubwa wa mawazo mbalimbali yatakayo kupelekea kuupata utajiri.

13. Kanuni ya kumi na tatu kuelekea utajiri  HISIA YA SITA
Mwandishi anailinganisha sixth sense (akili ya sita) kama lango Kwa Hekalu la Hekima
Uelewa wa akili ya sita unakuja tu kwa kutafakari, kupitia maendeleo ya akili kutoka ndani.Mara tu unapofahamu hisia ya sita, utakuwa na uwezo wa kupokea maonyo juu ya hatari zinazokuja kwa wakati ili kuziepuka na kujulishwa fursa za kukumbatia.Akili ya sita haitaweza kamwe kufanya kazi ikiwa mawazo, shaka, na woga zitabaki akilini mwako.
Hofu 6 za msingi ni; Umasikini, Ukosoaji, Afya mbaya, Upotevu wa upendo, uzee, Kifo anaongezea ya saba ambayo ni  ushawishi mbaya. Ili kujikinga na adui huyu, kama watu wote wanaokusanya utajiri mkubwa, lazima uweke matumizi yako ya nguvu kila wakati, hadi ujenge kinga dhidi ya ushawishi mbaya katika akili yako mwenyewe,Tafuta kwa hiari kampuni ya watu wanaokushawishi kufikiria na kutenda kwa mtazamo mzuri, na Tumia nguvu yako ya dhabiti kupata udhibiti wa mawazo yako na ushawishi akili yako ndogo.
Tambua hofu ni hali ya akili tu. Imewekwa chini ya udhibiti na mwelekeo. Tumia maarifa haya kwa faida yako.

MWISHO KWA MAELEZO ZAIDI NA JINSI YA KUJIUNGA NA GRUOP LETU TUMA UJUMBE KUPITIA 0767702659 LACKIUS ROBERT.
KARIBU TUJIFUNZE ZAIDI au bonyeza link hii https://t.me/SOMAONLINETELEGRAM

No comments:

Post a Comment