Karibu katika mwendelezo wa uchambuzi wa kitabu cha Rich dad Poor dad chake Robert Kiyosaki.
KAZI
KAZI
3. SOMO LA PILI: KWANINI
TUNAFUNDISHA ELIMU YA FEDHA?
Katika
sura hii Robert Kiyosaki anaelezea zaidi kwamba rafiki yake Mike alichukua mali
za baba yake na akazitunza vizuri mpaka kuwa na mafanikio.Robert na mke wake
Kim walistaafu mwaka 1996 akiwa na umri wa miaka 47 na mke wake 37 .Kustaafu
kwao hakukumanisha kuwa waliacha kufanya kazi .Ila kipindi hicho walikuwa
wanafanya kazi zao zingine na pesa
ilikuwa inaingia na yeye aliona hali hiyo kama uhuru wa kifedha.Hivyo mike
alichagua kutumia ufalme wa baba yake na Robert alichagua kustaafu.
Watu
wengi wanakuwa wakiniuliza kuwa ninapataje pesa ? Na wao wanaweza wakaanzia wapi ? na nini siri
ya mafanikio nimekuwa nikiwajibu hivi:
Kama
wako tayali kuendana na mabadiliko na kufungua akili yao pamoja na kujifunza
watakuwa matajiri na matajiri kwa sababu fedha bila kuwa na ufahamu wake
itapotea bule.
Ili
kuwa milionea haijalishi kiasi gani unapata
bali kiasi gani umewekeza na kiasi gani unazalisha kwa sasa.Ukitaka kuwa
tajiri unapaswa kuwa na elimu ya fedha( financial literacy).Ndio maana mimi
na Mike tunauwezo mzuri wa kuhifadhi
pesa zetu ,tuna msingi mzuri wa fedha tuliofundishwa na Baba yetu tajiri.
Shule
zetu hazituandalii msingi mzuri kuhusu fedha bali zinatuandalia ufaulu mzuri na
kupata kazi yenye mshahara mzuri.Kama unataka kuwa tajiri lazima ujue
kutofautisha faida (asset) na hasara ( liability).Asset ni kitu kinachoingiza fedha mfukoni lakini liability ni kitu kinachotoa fedha
mfukoni.Matajiri wanahifadhi vitu vinavyowaletea faida lakini watu wa kipato cha
kati wanamiliki vitu ambavyo haviwaingizii faida wanadhani ni faida kama mchoro
unavyoonesha.
Ø Mchanganuo
wa mapato kwa mtu masikini
MAPATO
|
MSHAHARA
|
MATUMIZI
Kama
vile
Kodi
ya serikali
Chakula
mavazi ,kodi ya nyumba n.k
|
Faida
na hasara kwa mtu maskini hapo ni kwamba fedha inaimgia na kutoka hakuna unachobakiza.
Ø Mchanganuo
wa mtu wa kipato cha kati
MAPATO
|
MSHAHARA
|
MATUMIZI KAMA :
Kodi
ya nyumba
,shule,malipo
ya rehani.
|
MADENI kama; Mkopo wa
nyumba,shule na kadi za benki.
Ø Mchanaganuo
wa kipato cha tajiri
MAPATO(income)
KAMA:
Mgawanyo
wa riba.
|
MATUMIZI(expances)
Assert(faida) Liability
(hasara)
Hisa ,Nyumba.
Malipo ya
kodi rehani,Kadi za Benki.
|
Kwa
ufupi ili kuwa tajiri au kupata uhuru wa
kifedha inabidi mapato yako yawe chini ya matumizi yako.Ukiangalia michanganuo mitatu hapo juu utakuja kugundua kwamba maskini pamoja na mtu
wa kipato cha kati bado wako kwenye madeni kipato chao havilingani na matumizi
yao .Lakini tajiri kipato chake na matumizi yake havijapishana ndiyo maana matajiri wataendelea kuwa matajiri
na maskini na watu wa kipato cha kati watazidi kuwa masikini.
4. SOMO LA TATU : FANYA SHUGHULI
ZAKO MWENYEWE.
Unapokuwa
unamfanyia kazi mtu mwisho wa siku hautatoka na chochote atabaki nacho
yeye,kama unahitahi kuacha mapambano ya kifedha fanya kazi zako mwenyewe,mfano
ukiangalia wafanya kazi benki,wanasayansi wahasibu wote hawa shule imewaandaa
kufanya kazi nakupata kupata mshahara lakini baada ya kustaafu hawabaki na kitu
chochote.
·
Utaalamu wako kipato chako
·
Mali zako kipato chako.
Kuna
utofauti mkubwa kati ya utaalamu wako wa kazini na shughuli zako mwenyewe mfano
Robert wakati anazungumza na
wafanayakazi wa benki aliwauliza hivi nyinyi shughuli zenu ni zipi ?, wakasema za kibenki,
mkimaliza inakuwaje wakasema tunaziacha.
Ukimlinganisha mtu mwenye shughuli zake
anaendelea kubaki nazo.Tatizo linaokumba wasomi wengi ni kwamba wanakuwa
walichokisomea, kama umesomea uhasibu utafanya kazi benki,kama umesomea mpishi
utakuwa mpishi kama umesomea sheria utakuwa jaji kama umesomea ualimu utakuwa
mwalimu na wengine hawajiongezi katika kufanya shuli zao wenyewe wanaendelea
kuwafanyia kazi na kuwatajirisha mabosi.
Ukitaka
kuwa tajiri fanya uwekezaji ambao utakuondoa kwenye madeni,vile vile watoto
wetu tuwaandalie mazingira mazuri ya kuwafundisha elimu ya fedha na jinsi ya
kufanya uwekezaji sahihi kama;
(i) Mfumo mzuri wa biashara ambao hata kama haupo
unajiendesha wenyewe (ii) Stock( hisa)
(iii) Bond( dhamana),(iv) Mutual
fund (mfuko wa pamoja),(v) Motes( vidokezo),(vi) Royalities intellectual
property such as music, scripts, patents,(vii) Real estate( Mali isiyohamisika)mfano
nyumba.
Kama
mtoto akifundishwa hivi pia na mzazi akazingatia vitu hivi kwa kufanya kazi zake
mwenyewe tayali atakuwa na uwezo mkubwa wakupata uhuru wa kifedha.
5. SOMO LA NNE: HISTORIA YA KODI NA NGUVU YA MASHIRIKA.
Mwandishi
anazungumzia kuwa kodi siku zote inawanyonya wazalishaji mali na kuwafaidisha
wasiokuwa wazalishaji mali ,Hii kwake anaona sio sawa matajiri siku zote
hutafuta namna ya kukwepa kulipa kodi lakini maskini wanalipa kodi kubwa sana
kuliko hata kipato chao.
Pia
anasema masikini wanaendeshwa na mashirika wakati matajiri wanayaendesha mashirika
na wanayatumia kupata pesa,Wanatumia mashirika haya kulinda kuboresha vitega
uchumi vyao. Wanayatumia mashirika haya kukwepa kodi,Wanajua kuyadanganya
mashirika na kupata pesa zaidi,Wanachukua pesa, wanalipa kodi, na kuishi kwa
pesa zilizobaki.Masikini wananyonywa na mashirika haya lakini hawajui kama
wananyonywa. Ili kuwa tajiri ni mhimu kila mtu akaanzisha biashara ya kwake.
lazima kila mtu ainue IQ yake ya uchumi, ujuzi wa soko, utunzanji wa fedha na
uwekezaji.Pia anasema
Ninaposema
shirika ni idara maalumu mfano kampuni inayoundwa ili kushughulikia usimamizi
na utekelezajiwa shughuli maalumu kama vile za kibiashara,Mfano hapa Tanzania
kuna Shirika la Reli ,Shirika la habari n.k.
Mwandishi
anajaribu kelezea kidogo kuhusu kuanziswa kwa kodi nchini marekani na uingereza
anasema kodi hizo zilianzishwa kwa lengo kubwa la kupambana na hasara
iliyojitokeza kutokna na uwepo wa vita.Katika swala la kodi kuna watu wanajiuliza
mbona maskini na tajiri wanalipa kodi sawa kwanini matajiri wasilipe kodi
tofauti na maskini?.Anasema matajiri wanajua vizuri nguvu ya ushirika na
wanawekeza huko kuliko watu wa kipato cha kati na maskini.
Nikikumbuka
katika somo la kwanza kuhusu nguvu, unapofanya kazi kupata pesa unakuwa huna
nguvu ya kujiongoza mwenyewe bali unampa nguvu mwajiri wako , lakini pesa
inapokufanyia kazi unakuwa na uwezo wa kuithibiti ipasavyo.Baba msomi alinambia
niende nikafanye kazi kwenye shirika kubwa nipate pesa zaidi lakini baba Tajiri
anasema kwanini nisiwe nasimamia mshirika yangu? ,Nilipokuwa mdogo sikuwahi
kumuelewa, nilianza kumuelewa nilipofikisha miaka 20 ,na ilipofika mwaka 1974
wakati bado ni mwajiriwa nilifungua kampuni yangu na nilikuwa nawafariji
wafanyakazi wangu.
Ninawakumbusha
watu kuwa elimu ya msingi wa fedha
imeundwa na maarifa kutoka makundi manne ambayo ni;
(i) Uhasibu, Ambayo ninaiita ujuzi wa kifedha
,Ujuzi muhimu ukiwa unataka kujenga msingi mzuri wa pesa zaidi unayoitaka. Huu ndio
upande wa kushoto wa ubongo. Ujuzi wa kifedha ni uwezo wa kusoma na kuelewa taarifa
za kifedha , uwezo huu hukuruhusu kutambua nguvu na udhaifu wa biashara yoyote.
(ii) Uwekezaji, Ambayo ninaiita sayansi ya
utengenezaji pesa, hii inajumuisha
mikakati na kanuni za upataji pesa. Huu ndio upande wa kulia wa ubongo, au
upande wa ubunifu.
(iii)
Kulielewa soko, Sayansi ya usambazaji na uhitaji. Kuna haja ya kujua mambo haya
kiufundi kuhusu kulifahamu soko, ambayo huchochewa na hisia, Sababu
nyingine ya soko huu ni msingi au hali ya kiuchumi ya uwekezaji. Watu wengi
wanafikiria dhana za kuwekeza na kuelewa soko ni ngumu sana kwa watoto.
Wanashindwa kuona kwamba watoto ni vema
wakawa wanajua masomo hayo kiundani wakiwa bado watoto.
(iv) Sheria, Kwa mfano, kutumia shirika
lililofunikwa kwa ustadi wa kiufundi wa uhasibu, uwekezaji na uelewa wa masoko
yanaweza kusaidia ukuaji wa kifedha. Mtu aliye na maarifa ya faida ya ushuru na
ulinzi inayotolewa na shirika anaweza kupata utajiri haraka sana kuliko mtu
ambaye ni mfanyakazi au mmiliki wa biashara ndogo ndogo. Ni kama tofauti kati
ya mtu anayetembea na mtu anayeruka.
6. SOMO LA TANO: MATAJIRI
WANAWEKEZA KWENYE FEDHA.
Nimekuwa
nikifundisha tangu 1984 nimekuwa uzoefu mzuri na pia na kutoa taaluma niliyonayo.
Nilifundisha
maelfu ya watu binafsi na ninaona jambo moja katika sisi sote kuwa tuna uwezo
mkubwa, na sote tumebarikiwa na zawadi. Bado, jambo moja ambalo linashikilia
yote kwetu nyuma ni kiwango cha kujiona tunajua. Sio ukosefu mkubwa wa habari
za kiufundi ambayo zinatuzuia, lakini zaidi ukosefu wa kujiamini. Baadhi huathiriwa
zaidi kuliko wengine mara tu tukiacha shule, wengi wetu tunajua kuwa swala la
digrii za chuo kikuu au darasa zuri ndio zinahesabu mafanikio,kumbe unaweza
pata mafanikio makubwa kupitia elimu ambayo haukufundishwa shuleni.
Katika
uzoefu wangu wa kibinafsi, fikra zako za kifedha zinahitaji maarifa ya kiufundi
pia ujasiri. Ikiwa hofu ni kubwa sana, akili hukandamizwa. Katika madarasa
yangu nawasihi sana wanafunzi,jifunze kuchukua hatari, kuwa na ujasiri,
kuiruhusu akili zao zibadilishe woga huo kuwa nguvu na uzuri. Nilinafanya kazi
kwa wengine na nimegundua kwamba kwa watu wengi, wakati inakuja mada ya pesa,
wangeamua kucheza salama. Nimelazimika kuhoji maswali kama haya kama, Kwa nini
uchukue hatari? Kwa nini nijisumbue kukuza IQ yangu ya kifedha? Kwa nini niweke
fedha kusoma na kuandika?.
Kuna
mtu kama Bill Gates na kampuni zake
Microsoft zinazoundwa kila mwaka kote ulimwenguni na kote zinafanya kazi
vizuri ,sio kwamba yeye hana woga bali
anathubutu na kuwekeza kwenye pesa ili imsaidie baadae hivyo ni vema kufurahisha zaidi kuwa hai. Ningependa
kufurahi juu ya kutengeneza mamilioni kuliko kuwa na wasiwasi juu sio kupata
kipato. Kipindi hiki tulicho sasa ni kipindi cha kufurahisha zaidi mambo ambayo
hayajawahi kufanywa ndani ya historia ya ulimwengu, na tutafurahia zaidi endapo
tukiwekeza kwenye pesa.
Tutaendelea na sehemu sa Saba wakati mwingine.
karibu upate uchambuzi wa vitabu vingine ,nitumie ujumbe kupitia namba 0767702659 au email
maarifarobert@gmail.com.
Karibu tujifunze zaidi.
No comments:
Post a Comment