Wednesday, December 18, 2019

MBINU ZA MAFANIKIO NA LACKIUS ROBERT


UCHAMBUZI WA KUHUSU MAISHA NA MAFANIKIO NA  LACKIUS ROBERT
Zingatia haya machache yafuatayo

 TABIA YA KUBAGUA KAZI;
Hakuna binadamu aliyeumbwa kufanya kazi fulani na mwingine afanye kazi ile sote tunafanya kazi kuendana na maisha yetu yalivo.utfiti unaonesha kuwa asilimia 80% ya kushindwa kufikika kwa malengo kunachangiwa na sisi  mwenyewe katika fikra zetu yaani inner feeling halafu asilimia 20% ni Sababu za nje,matumaini yangu makubwa kwamba wengi wetu tunazitambua changamoto zinazotukabili kwa ambao tupo kwenye masomo tunatambua kwamba changamoto kama vile  ajira ipo tumeisikia hata wengi wetu  bado hatujaingia kwenye elimu ya juu na cha kushangaza ni kwamba baadhi yetu pesa tunazopewa  na wazazi wengine wnapewa na bodi lakini tunazitumia katika matumizi ambayo wakati mwingine yasiyo sahihi simanishi kwa wote ila kama unazitumia katika matumizi ambayo sio sahihi inakuhusu na tutambaua mlima ulio mbele yetu kwenda nyumabani kulima hautaki wakati pesa unazipata umazitumia vibaya je nani wa kulamiwa mzazi wako serekali au nafisi yako.nayaongea hayo maana nimewatazama vijana wengi wakiangaika baada ya kuhitimu masomo yao,huku wakilaumu sana.

Pia vijana wenzangu baada ya kuhitimu masomo kubagua kazi kunakuwepo wapo wengine wanaona kazi kama vile kuuza maji ,kupakia mizigo ni kazi ambazo anaona hazimfai kabisa tunashindwa kutambua kwamba hio pesa yenyewe tunayoitafuta haijawahi kumbagua mtu yeyote ndio maana utajiri auna ubaguzi utakuta vijana wengine miaka ishirini ana pesa za kutosha mzee mwenye miaka sitini au hamsini ana pesa za kubabaisha ,wzazee wengine wanapesa za kuosha wengine wamesoma wengine hata chekechekea hawajaenda lakini pesa anazo kwa hio vijana wenzangu swala la kubagua linatufanya tunabaki kuhangaika tu mijini na vijijini.Kinachoshangaza ni kwamba unamkuta kijana mwenzangu hana hata mia lakini ukimwambia njoo basi tukapige kibarua hata kusomba tofali kwa siku elfu saba au elfu kumi anakwambia hizo kazi sio za kwetu wapo wenye uwezo kwa kuzifanya ,na je! pesa na yenyewe ingesema mi nataka nishikwe na huyu Yule hafai ingekuwaje au kama ingewachagua wasomi tu,au ambao hawajasoma duniani tungeishi je?.

Vijana wenzangu ambao hatupo kwenye masomo ni mengi sana tunayaona pamoja na kuyasikia redio mbali mbali zinatangaza viongozi mbali mbali wanasema kuhusu namna gani vijana tuwe na maisha mazuri.Mimi nafurahi sana ninapowakuta vijana wanajishughulisha na shughuli kama vile biashara ndogo ndogo siku moja nilikuwa Ubungo nikakutana na kijana mmoja anabeba mizigo kwenye mkokoteni na kuzipereka sehemu tofauti kutegemea na wasafiri wanapoelekea nikabaatika kuzungumza nae kwa kina akanieleza jingi gani anavyopenda kazi yake licha ya kwamba pesa anayopata sio nyingi lakini mahitaji ya familia anayapata pia na kulipa kodi ya nyumba..

Changamoto yetu vijana wengi tunadharau kazi hasa hasa zile za kutumia nguvu nyingi lakini tukumbuke imeandikwa kila mtu atakula kwa jasho lake ,mbuzi anakula kulingana na urefu wa kamba yake ila tunashindwa kufanya mfano mdogo wa kuku,nafukili wengi tunamjua jinsi gani anavyotafuta chakula chake kwa kuparua parua huku asipopata wadudu anageukia pale pale upande wa pili na kupata wadudu na kuwala .Vijana tuchotaka kuona ni kupata kazi nyepesi nyepesi kwa hali hio hatutafka mbali tuutume ujana wetu kufanya kazi nzito juani wakati  huo tukitegema kuvuna mazao tukiwa kivulini Walen Buffet anasema’ kivuli cha mti uliokalia leo kuna mtu aliupanda’kwa hio tupande mbegu bora kwa ustawi wa maisha yetu. Kila mtu anaouwezo mkubwa wa kufanya kazi yoyote endapo akilegeza mwili na kururusu moyo kuwa na  amani kwa kila kazi iliyoko mbele yetu. .

ILE HARI YA TAMAA;
Hali ya kutamani kitu fualani haiepukiki kwa maisha ya mwanadamu yeyote maana kutoka na kutamani ndiko tuapata ushindani pengine mafaikio pia wapo wanaotamani wazaliwe kama wachezaji wakubwa kama hapa Tanzania Mbwana Samatta kina Msuva na wengineo,wasanii wakubwa kama Diamond ,Lady Jay Dee ,waamashishaji maarufu kama Eric Shigongo,Nanauka Antony Luvanda na wengineo wengi tamaa ya namna hio kama tukitamani na kuongeza juhudi inakuwa ni nzuri .Kiuharisia kila mwanadamu anapaswa kutamani  tama mbele mauti nyuma maana kutokana na kutamani ndipo tunapata namna ya kusogeza maisha yetu mbele tama ipo katika Nyanja tofauti maana kila mmoja wetu  ana namna anavyotamani. 

Tamaa ya moyo, yaani tama hii Kwetu vijana imekuwa ni tamaa ambayo wakati mwingine hutususumbua na kuharibu mipango yetu ya maisha 20% katika wimbo wa’’ tama mbaya’’ anasema moyo sifa yake kutamani tama ya moyo inaweza kukuweka matatani. Mara nyingi tumekuwa tunatamani mambo makubwa kuliko uwezo wetu kama vile nyumba magari  nyingi wakati hatujaweka njia za kupata vitu hivyo na tamaa hiyo mara nyingi inapelekea kuhahirisha baadhi ya vitu tunavyokuwa tumeweka tumeona vijana wawili waliokuwa na mpango wa kujenga nyumba na mmoja wao akatamani ashobokewe na mabinti hadi akaamua kununua pikipiki ambayo hakudumu nayo muda mrefu na tama yake ilimponza.

Pia kuona kitu chochote kizuri moyo unakitamani kwetu vijana unamwona binti au mvulana mzuri moyo unamtani hadi akili nzima kichwani ivnavurugika unatamani kupata japo hata dakika kadhaa za kuzungumza nae ,uwepo pia wa mitandao ya kijamii umechangia sana vijana wengi kutamani sana maana kuna wengine wanapost picha zinazoonesha nguo za ndani ,aina mbalimbali za mitindo mara nywele,nguo n.k na sisi vijana tukiona wanapata comments na likes nyingi tunapata shauku ata kubadilisha miili yet undo wengine tunaona wanajichubua wananyoa mitindo tofati ya nywele na vijana wa kuime kutoboa masikio lengo ni kutaamani kuwa kama wale anaowaona lakini tutambue vijana  kusimama imara na kutunza miili yetu ni jambo ambalo linaleta heshima hata kwa jamii inayotuzunguka.

Tamaa ya pesa,jambo lisilo napingamizi kwamba kila mmoja wetu anataka awe na pesa za kutosha ili kujikimu kimaisha tama ya pesa hauwezi kuikwepa hata siku moja wengi tunaishia tu kutamani lakini hatuweki mipango madhubuti ya kupata pesa hizo inafika hatua wengi wetu wanaingia kwenye wizi,unyanganyi kwa watu wanoonekana wanapesa ,mali lengo ni kutaka kuwafanya hao vijana waingie katika ulimwengu wa matajiri.

Kuwa UNSTOPPABLE maana yake usitishiwe au kuyumbishwa na vitu vinavyoonekana havina tija kwa maisha yako ya kila siku,vijana tunyanyuke na kufanya kazi kwa bidii pes ipo ukiitafuta utaipata lakini kuendelea kulalamika pesa hakuna vyuma vimekaza hakutatusaidia kumbuka wanasema hata safari ya maili elfu moja huanza na hatua moja Yule tajiri tunayemuona anapesa za kutosha naye alianza na shilingi 100 na kuendelea je mimi na wewe tunataka tuanzie shilingi ngapi ?.

Jambo la muhimu kuzuia tama ya pesa kutusumbua tuweke ratiba maalumu ya kuwa tunatunza akiba kila baada ya kupata kiasi fuani cha pesa haijarishi tumetunza kiasi gani baada ya muda alienza na mia moja tutakuwa katika harakati za kumfikia .Natambua changamoto zipo kila siku na hazitaisha lakini najiuliza kama baadhi ya vijana wenzetu wamefaulu kuzishinda changamoto hizo wakawa unstoppable kwa nini mimi na wewe? Je! Wao wana miguu,macho na mikono  zaidi ya mbili? .

Tufanye maamuzi sasa wakati ndio huu, katika kutamani kupata pesa Elieshi Lema katika kitabu cha ‘’In the Belly of Dar es salaam ‘’ amejaribu kuonesha baadhi ya vijana wanaotamani kuja mjini wakifikilia kuna maisha mepesi na kukimbia maisha yao ya kijiji baada ya kufika mjini wanakuta ni tofauti kabisa na matarajio waloyawaza pindi wapo nyumbani baada ya kuona maisha yamekuwa magumu huanza kujiingiza katika matendo mabaya ikiweo kufanya ukahaba wizi n.k.

Tamaa hii mara nyingi inachochewa sana na makundi ya marafiki tunaokuwa nao nimesoma stori kadhaa za madada wenye kutamamani pesa za haraka mpaka wakajiingiza kwenye biashara ya kuuza mwili,vijana wengi wa kiume kuishia kucheza kamali lengo ni kutaka kuwa na pesa alizonzo Fulani katika kundi lao na hali hii ya tamaa humfanya mambo yasiyo na tija kubwa kwa maisha ya badae mfano madwa ya kulevya, mtu anakosa amani anafanya kazi kufa na kupona mpaka apate kama cha mwenzake badala ya hizo nguvu kuziweka katika maendeleo ambayo yatanufaisha familia yake na taifa kwa ujumla.

Mawasiliano zaidi 0767702659 Lackius Robert karibu sana. Ili kuendelea kupata chambuzi mbali za vitabu bonyeza link hii ili uendelee kupata ucambuzi wa vitabu kwa lugha ya kiswahili.
htthttps://t.me/SOMAONLINETELEGRAM




Uchambuzi wa kitabu cha How successful people think chake John Maxwell


MORNING MOTIVATION DIARY 
PRESENT: UCHAMBUZI WA KITABU
JINA: HOW SUCCESSFUL PEOPLE THINK: Change your thinking,change your life
JINSI WATU WALIOFANIKIWA HUFIKIRIA: Badilisha fikra zako, Badilisha maisha yako.
MWANDISHI : JOHN C.MAXWELL
UTANGULIZI

Wafikiriaji wazuri daima wanaangalia mahitaji,Wanatambua kazi zao za kila siku na kila wakati ni watu wanaojua kwanini wao ni mabosi.Mara zote hutatua shida zinazojitokeza katika sehemu wanazoziongoza iwe ni kwenye kampuni au la kamwe hawapungukiwi na maini jinsi kuendesha uongozi wao,wanakuwa na fikiri za mbali kuhusu kuwa na kesho ambayo ni bora.
Mwandishi John Maxwell anasema ,Nimejifunza zaidi ya miaka  arobaini na kugundua kuwa kinachowatofautisha waliofanikiwa na wasiofanikiwa ni namna wanavyofikiri,waliofanikiwa mara zote wanajua umuhumu wa kujifunza zaidi na uzidi kujifunza ukilinganisha na watu wasio na mafanikio.

Kwanini unapaswa kubadili fikra zako?
Japokuwa kubadili fikra zako sio rahisi lakini ukiamua unazweza lakini unapswa ujue kwamba kubadili fikra hakuji automatiki lazima kuwe na kichocheo ,hivyo  kubadili fikra zako kunakusaidia kutatua matatizo mbalimbali na kukutengengenezea fursa.Pia unapelekea kuruhusu hisia zako kufanya kazi vizuri maana mfumo uwezo wetu wa kufanya jambo lolote unaanzia katika fikra zetu ndipo matendo yanafatia.Ufikiriaji mzuri unasaidia sana mtu kuyafikia malengo aliyoyaweka katika kazi zake ikiwemo wale anaowaongoza.
Ilii uweze kuboresha zaidi ufikiriaji wako
Tafuta sehemu tulivu ambayo haina mizunguko ya watu ukae utulie na uanze kutafakari kuhusu yale unayoyatamani kuyafanya baada ya kuyafikiria vizuri na kuyaweka katika mipangilio mizuri hatua kubwa inayofuata ni kuyaweka katika matendo.Jambo la kuzigatia ni kuwa unafanya hivyo mara nyingi ili kuweza kuuzoesha ubongo wako ufanye kazi zaidi na zaidi mafanikio yako yanaongozwa na fikra zako.

Ndugu karibu tuzichambue sura moja baada ya nyingine ni  matumaini kuwa  utafurahia pamoja na kuchukua hatua baada ya kufika mwisho wa uchambuzi wa  kitabu hiki.
SURA YA KWANZA

Tengeneza picha kubwa ya kufikiria
David SCHWARTZ aliwahi kusema "Pale ambapo mafanikio yanahusika, watu hawapimwi kwa nchi, pesa walizonazo au digrii za chuo kikuu, au asili ya familia zao bali hupimwa kwa ukubwa wa mawazo na yao. "
Unapokuwa umefikiri katika mapana ya picha kubwa ni njia ambayo itakupa ufanisi wa fikra zako. Sifa kubwa waliyonayo watu wanaofikiri kwa mapana ya picha kubwa ni kwamba daima huwa hawaridhiki na hali inayowakabili muda wote bali wanakuwa macho kwa ajili ya fursa mpya. Watu hawa wanajifunza kila mara kutoka kwa watu wengine na hivyo wanafanya kazi kwa bidii na ubunifu katika shughuli zao kila siku. Watu hawa wanatambua nguvu kubwa iliyopo kwenye usikivu kutoka kwa wengine kuliko kuwa wazungumzaji wakubwa. Pia, watu hawa muda wote wanatazama mbali malengo yao makubwa ni kutafuta fursa mpya ili wazifanyie kazi.
Kwa nini utengeneze picha kubwa ya kufikiria?
·         Kufikiria mapana yenye picha Kubwa inakusaidia kuongoza,Kama kiongozi unapokuwa na picha kubwa katika ufikiriaji wako unakuwa na maono makubwa kabla ya wengine kuyaona,unakuwa unawaza ya kesho kabla yao,unakuwa na mitazamo ya kule mnakoenda tofauti na wao waliyonayo.Ikiwa ni kujenga barabara, kupanga safari za kikazi katika uongozi, mawazo ya picha kubwa hukuruhusu kufurahia mafanikio zaidi. Watu ambao wanaangalia kila wakati picha nzima wana nafasi nzuri ya kufanikiwa kwa juhudi yoyote.
·         Kufikiria picha katika ukubwa Kunakupeleka kwenye mahali ulipolenga,Ili kufanya vitu vizuri, unahitaji kufikiria jambo katika upana wake ikiwemo kulielewa na kulifanyia kazi pasipo kusuburia.
·         Kufikiria jambo  kwa upana kunakusaidia kuona wengine wanapoona ,Moja kati ya ujuzi ambao mtu yeyote anahitaji kuwa nao ni uwezo wa kuona wengine wanapoona ,kwa kufanya hivyo hujikuta anawahudumia wateja wake vizuri tena kwa kuwaridhisha lakini hali hii inaambatana na ufikiriaji mzuri  unaoendana na kuwa unatafakari mambo katika ukubwa.
·         Kufikiri jambo kwa upana kunasaidia kuboresha ushirikiano kwa kufanya kazi kwa pamoja na kuboresha mahusiano ikiwemo kusaidia na hii upendeza watu wanaofikiria mambo kwa upana zaidi wanapokutana.
Hivyo ili kuweza kuboresha uwezo wako wa kufikiri jambo kwa upana zaidi unatakiwa kujifunza kutoka katika kila uzoefu unaopitia au pale unapokuwa unafanya kazi na wengine mkabadirishana mawazo ya hapa na pale.Unapokuwa na wazo sahihi, unatakiwa uwashirikishe watu sahihi kwa ajili ya wazo husika, wazo pia lazima lishirikishwe katika mazingira sahihi, muda pia unatakiwa uwe sahihi.

SWALI : Je nafikiri zaidi yangu,ulimwengu wangu ili niweze kushughulikia maoni kwa mtazamo kamili?.Karibu upate sura ya pili mpaka mwisho wa kitabu hiki

Kupata uchambuzi zaidi wa kitabu hiki tuwasiliane kupitia 0767702659 Lackius Robert

Wednesday, December 04, 2019

Uchambuzi wa kitabu cha Ishinde tabia ya kughairisha mambo chake Joel Nanauka


MORNING MOTIVATION DIARY 
PRESENT: UCHAMBUZI WA KITABU
JINA: OVER COMING PROCRASTINATION,  ISHINDE TABIA YA KUGHAIRISHA MAMBO
MWANDISHI : JOEL NANAUKA.
UTANGULIZI:

Moja ya sababu kubwa ambayo inawafanya wengi kushindwa kutimiza malengo yao kwa wakati ni kughairisha mambo.Wengi wetu tunaseam ngoja niache kidogo ntamalizia baadae lakini baadae inapofika tunajikuta tayali tuna mambo mengine ya kufanya ilo tunalisahau.
Mwandishi Nanauka anaanza kwa kuuliza “Unakumbuka wakati watu wametangaziwa kujisajili kwaajili ya kupiga kura? Unakumbuka watu walivyotangaziwa kuhusu usajili wa vitambulisho vya utaifa? Ni siku gani watu walijaa zaidi? Bila shaka, utakumbuka ni siku ya mwisho hata kama waliliona tangazo. Kuna watu kila siku wanatuma maombi ya kazi siku ya mwisho hata kama waliliona tangazo hilo miezi miwili kabla. Kuna watu kila wakati watatuma ripoti yao siku ya mwisho, kuna watu kila wakati kazi waliyopewa kufanya wataiwasilisha dakika za mwisho”.Bila kujua madhara mkubwa yanayotokea baadae ,wengi wao hujikuta katika hali ya kuwa na stress(msongo wa mawazo) maana ata kazi wanapozifanya zinakuwa hazina ubora mzuri na hufanywa kwa kiwango cha chini kabisa na hali hii utokana na tabia ya kughairisha.Anasema alimia 95 ya wazee walipoojiwa walisema tunajuta kwa kughairisha mambo mengi katika maisha yetu ambayo tungeyafanya basi tungekuwa mbali zaidi.Huo ndio ukweli watu wengi wameghairisha mambo mengi tena ya msingi na kujikuta hawawezi kuyafanya tena.

Ndugu karibu tuzichambue sura moja baada ya nyingine ni  matumaini kuwa  utafurahia pamoja na kuchukua hatua baada ya kufika mwisho wa uchambuzi wa  kitabu hiki.

SURA YA KWANZA
Kwa nini watu wanaghairisha mambo?,utafiti wa kisayansi kuhusu kughairisha mambo.

Utafiti uliofanywa na William James ambaye ni mtaalamu wa saikolojia uliochapishwa katika jarida la sayansi ya saikolojia mwaka  1997 akishirikiana na Dianne Tice ambao uliwahusisha wanafunzi kutoka chuo kikuu cha Western Reserve uligundua kwamba wanafunzi waliokuwa wanaghairisha walikuwa na msongo wa mawazo kuliko wanafunzi wasioghairisha hali hii ilikuwa inatokea hasa hasa katika ukusanyaji wa kazi(assignment) kwa mwalimu husika.Wakati wanafanya hivyo wanakuwa hawaoni Kama ni tatizo lakini baadae linakuja kuwa tatizo ,na mwishowe walijikuta hata kazi zao hazina ubora ukilinganisha na wanafunzi amabo walikuwa hawaghairishi mambo.

Mwandishi amebainisha taswira halisi katika maeneo ya kazi. Anasema wapo wafanyakazi ambao hawapendi kutekeleza kazi zao kwa wakati badala yake wanasubiri hadi dakika za mwisho ndipo waanze kuhaha huko na huko. Kimsingi tabia hizi zinazozungumzwa zinawagusa watu wa kila kaliba. Haijalishi umri wala nasaba au jinsia, Unaweza ukachukua daftari lako kuandika, ama ripoti yako ama hata kusoma kitabu, ukaamua kuwa unafanya unachotaka kwa nusu saa bila kuyumbishwa na kitu chochote, ghafla baada ya dakika 10 unajikuta nunashika simu na unasema ngoja niangalie meseji, kuja kushtuka unajikuta umeshatumia takribani nusu saa kuperuzi mitandao na hamu ya kuendelea na kazi uliyokuwa unaifanya inapotea kabisa. Ama wakati mwingine unasema ngoja niangalie TV kidogo kisha nitalala ama nitasoma kidogo, kuja kugundua unakuwa imeshafika saa 7 usiku na umeshindwa kuondoka kwenye TV yako.

Katika muktadha huo mwandishi anakumbusha kuwa wapo watu wanaoishi kwa kuahirisha. Wengine ambao hadi wakumbushwe ndipo hutekeleza jambo fulani. Wapo watu ambao hawezi kujikita kwenye eneo husika. 

Mwandishi anatumia utafiti wa Profesa Joseph Ferrari ambaye aligundua kuwa takribani asilimia 20 ya watu duniani ni waahirishaji wakubwa wa mambo yao,ambapo ufafanuzi wake umejikita katika mifumo miwili iliyopo kwenye ubongo kwa jinsi inavyoshindana.
Kuna mfumo unaitwa Limbic system huu una sehemu ambayo ndiyo unahusika na wewe kujisikia raha unapofanya jambo Fulani,mfano unapokula chakula kizuri,unapofanya tendo la ndoa na mengineyo.

Mfumo wa Prefrontal Cortex huu ni mfumo upo nyuma ya kipaji chako cha uso kazi yake kubwa ni kukuongoza katika kufanuya maamuzi mbali mbali.Huu ndio mfumo unaokusaidia kujua kipi kizuri na kipi kibaya kupitia tathimini hiyo unaweza kufanya tathimini ya kila kitendo amabacho unakifanya na kupima madhara yake.Hiyo ndiyo vita inayoendelea katika ubongo wako katika mambo mbalimbali unayotaka kufanya.
Unaporuhusu mfumo wa limbic kuwa na nguvu kuliko prefrontal cortex ambao ndio una uwezo wa kufanya maamuzi basi utajikuta unakosa hamasa na kuwa mgairishaji mzuri ambapo madhara yake ni kukosa nidhamu ya muda, kuhisi una mambo mengi yasiyokwisha sababu ya kutotekeleza kwa wakati na kulimbikiza majukumu ,utakosa hamasa ya kufanya jambo pia  utakosa  kuweka vipaumbele.
karibu ujipatie sura ya pili na kuendelea .....

Mchambuzi LACKIUS ROBERT karibu kwa mawasiliano zaidi 0767702659 email maarifarobert@gmail.com Kila kitabu kimoja kilichochochambuliwa ni shilingi 1000/= uchambuzi upo katika  mfumo wa PDF kupitia email ,Whatsup na telegram

UCHAMBUZI WA KITABU CHA EAT THAT FROG


MORNING MOTIVATION DIARY 
PRESENT: UCHAMBUZI WA KITABU
JINA: EAT THAT FROG, 21  GREAT WAYS TO STOP  PROCRASTINATING AND  GET MORE DONE IN LESS TIME. KULA HUYO CHURA ,NJIA 21 ZA KUEPUKA UGHAIRISHAJI NA KUFANYA MENGI KWA MUDA MFUPI.
MWANDISHI: BRIAN TRACY.
UTANGULIZI:

Brian Trace ni mwalimu mwenye uzoefu sana katika eneo la mafanikio. Baadhi ya mambo mengi ambayo Brian anatushirikisha ni yale ambayo amekuwa akijifunza, kisha anayafanyia kazi yeye binafsi na ndipo anatushirikisha kupitia vitabu vyake. Katika kitabu hiki ametushirikisha namna ya kupambana na hali ya kuahirisha mambo uliyopanga kuyafanya.
Ukweli kuhusu Chura
Mark Twain aliwahi kusema jambo kubwa unalopaswa kufanya kila asubuhi ni kula chura moja kwa moja."Chura" wako ndiye kazi yako kubwa na muhimu zaidi, ndio iliyo na uwezekano wa kuchelewesha ikiwa hautafanya jambo fulani juu yake. Pia ni kazi moja ambayo inaweza kuwa na athari nzuri zaidi maisha yako yote.
Sheria ya kwanza ya kula chura ni, "Kama utatakiwa kula vyura wawili, kula mbaya kwanza aliyebaki mmalizie baadae " ,Hii ni njia nyingine ya kusema kwamba, ikiwa una kazi mbili muhimu mbele yako, anza na kazi kubwa, ngumu na muhimu zaidi kwanza. Jiridhishe mwenyewe kuanza mara moja na kisha kuendelea mpaka kazi imekamilika kabla ya kuendelea na kitu kingine.Fikiria hii kama "jaribio.", Kataa jaribu la kuanza na kazi rahisi .
Sheria ya pili ya kula chura ni, "Ikiwa itabidi kula chura moja kwa moja, hailipi kukaa na kuiangalia kwa muda mrefu sana. " Ufunguo wa kufikia viwango vya juu vya utendaji na tija ni kwako kukuza tabia ya maisha yako yote ya kushughulikia kazi yako kuu kwanza kitu kila asubuhi. Lazima uendeleze utaratibu wa "Kula yako chura "kabla ya kufanya kitu kingine chochote, na bila kuchukua muda mwingi kufikiria juu yake.
Ndugu karibu tuzichambue sura moja baada ya nyingine ni matumaini kuwa  utafurahia pamoja na kuchukua hatua baada ya kufika mwisho wa uchambuzi wa  kitabu hiki.


SURA YA KWANZA,
Panga ratiba
Napoleon Hill aliwahi kusema"Kuna sifa moja ambayo mtu anayependa  kushinda anapaswa kuwa nayo , nayo ni kuweka kusudi  na ujuzi wa kile kitu ambacho ana hamu ya kukifanikisha. ”
Kabla ya kuamua kumla "chura" wako ili uendelee na kazi, lazima uamue unataka kufikia wapi kwenye  maisha yako.
Watu wengi wanashindwa kuyafikia malengo yao kwa sababu wanakosa motisha ya kufanya kazi ,kwa sababu hawana mwongozo ulio imara katika kuyafikia malengo waliyoweka.Utafiti unaonesha kuwa asilimia 3 ya walioweka malengo ndio waliofanikisha na wengine asilimia 97 walishindwa kuyafanikisha. Kuna hatua saba kama unahitaji kufikia malengo yako inabidi uzifahamu na kuzizingatia :
Hatua ya 1.Amua unataka uwe nani ,kaa chini tafakari chagua eneo ambalo unaona linakufaa lifanyie kazi.Steven Covey aliwahi kusema’’ kabla hujaamza kupanda ngazi ya mafanikio hakikisha ,ngazi imenininginia katika sehemu sahihi ya jengo’’
Hatua ya 2.Andika shehemu,Chukua kipande cha karatasi andika malengo yako ,wakati unaandika hakikisha unaandika malengounayoweza kutimizika ,yanayoonekana na kueleweka maana kuwa na malengo yasiyoandikiwa kunakupoteza.
Hatua ya 3.weka ukomo wa malengo yako,Maamuzi au malengo yasiyo na ukomo yanakuwa hayana uharaka ,hivyo unapopanga malengo hakikisha yanakuwa na ukomo ili kuepusha kughairisha mara kwa mara.
Hatua ya 4.Andika vitu vyote ambavyo unahisi ukiwa navyo vinaweza kukusaidia kuyafikia malengo yako.
Hatua ya 5. Pangilia vizuri mahitaji yako,weka vipaumbele/ pangilia vitu vya msingi sana unavyohitji ikifatiwa na vitu vingine amabvyo sio vya msingi sana.
Hatua ya 6. Chukua hatua,Fanya chochote, Mpango wa wastani uliotekelezwa kwa nguvu ni bora zaidi kuliko mpango wa kipaji ambao hakuna kitu kinafanyika .
Hatua ya 7.Amua  kufanya jambo moja kila siku lililo kwenye lengo lako,jitahidi kuzidi kujifunza zaidi na zaidi.

KUNA NGUVU KUBWA YA KUANDIKA MALENGO
Malengo ya maandishi yaliyo wazi yana athari nzuri kwa mawazo yako maana yanakuhamasisha na kukuchochea kuchukua hatua. Malengo ni mafuta katika tanuru ya mafanikio. Fikiria juu ya malengo yako na kuyapitia kila siku,Kila asubuhi baada ya kuamka, chukua hatua juu ya kazi muhimu zaidi unayoweza kukamilisha kufikia lengo lako muhimu zaidi kwa sasa.
SWALI:Je ni malengo yapi uliyojiwekea ili kufikia ndoto yako?.

Uchambuzi umefanywa na Lackius Robert kwa mawasiliano zaii 0767702659au maarifarobert@gmail.com

karibu  utatumiwa kwa njia ya PDF kupia whatsup,email,au tegegram.