Furaha
ni utulivu ulio ndani ya nafsi ya mtu mwenyewe,mara nyingi msingi wa Furaha
uleteleza utulivu wa Mwili na Roho ambavyo uleta matumaini na upendo kwa ndani
ya nafsi ya mtu.
Wakati
mwigine ili kuipata vema kukaa na watu wanaokupa furaha na kufanya
mambo yanayokupa furaha, . Watu wengi wanakosa furaha na amani na kujaa na
msongo wa mawazo katika maisha yao ya kila siku hasa makazini, majumbani,
kifamilia.
Kama unaamini kuwa unakosa furaha
kutokana na ugumu wa maisha, haujapata kazi, unasumbuliwa na mahusiano, umefeli kwenye masomo, umetengwa kwenye familia, unatafuta mtoto lakini hupati
na mengine kadha wa kadha inabidi ubadilike
kwani hata ukifanikiwa kuvipata vitu hivyo unavyovihitaji kamwe furaha yako
haiwezi kukamilika kutoka na tabia za asili za binadamu.
Msomaji
wa BLOG Hii Naomba nikushirikishe kidogo umuhimu kwa kuwa na furaha maishani;
Kuwa na furaha kunalinda moyo wako
Utafiti
unaonesha kuwa asili ya upendo na furaha siyo moyoni lakini husaidia kuulinda
huku ikibainika kuwepo kwa uhusiano baina ya furaha na vipimo vingine vya afya
ya moyo kama vile muda unaotumika wakati wa pigo moja la moyo na lingine na
kuzilinganisha na hatari kadhaa za magonjwa ya moyo.
Furaha huzuia mkazo
Makazo yaani sterss hausababishi matatizo ya kisaikolojia pekee bali pia husababisha
mabadiliko ya kibiology katika homoni zetu na shinikizo la damu. Furaha
inatajwa kupoza hasira za athari hizi na wakati mwingine kutusaidia kurudi
katika hali ya kawaida kwa haraka.
VITU
VYA KUEPUKA
Hali ya kukata tamaaa,
Walio
wengi hali hii imetukumba sana na tumeikosa furaha lakini ili uweze kuwa na furaha ya kudumu epuka kukata
tamaa au kukatishwa tamaa na mtu, kwa sababu kitendo cha kuruhusu kukataa tamaa
ni hatua ya mwisho ambayo hauna uwezo wowote wa kujitoa.Kamwe usiruhusu hali
hiyo jitahidi kuishi kwenye mtazamo chanya muda wote kuwa utafanikiwa kila
jambo unalopigania hata kama ukifeli usikate tamaa utayashinda.
Epuka kutoridhika,
Katika
maisha hakuna hatua ambayo mwanadamu utafika na kusema kuwa umeridhika kwa
maana hata mwandamu apewe kitu gani hakuna wakati atakaposema inatosha.Wengi
wamepoteza furaha kutokana na kutoridhika,akipata kitu hiki anataka kingine . Simaanishi
watu waridhike nachomanisha kiridhika na
unachokipata kutegemeana na hali ya kipato chako.Mfano kama auna uwezo wa kunua
gari na unatarajia upate furaha baada ya kupata gari itachukua muda hio furaha
yako kuipata kama ukifeli usikate tamaa utayashinda.
Ni matumaini yangu kwamba umeweza kuongeza kidogo uelewa namna furaha ilivyo bora katika maisha yetu.
Kauli za washindi nikwamba hawakubali kuikosa furaha .Je mimi na wewe tunaikosaje kwa mfano?.
''Ushindi upo mikononi mwako kwa kuwa umebarikiwa''
Kwa maoni na ushauri maarifarobert@gmail.com
Instagram @lackiusrobert
KARIBU.