" Siku moja Mbwa Mwitu alikuwa katika harakati zake za kutafuta chakula msituni. Alikutana na kundi
kubwa la Digidigi. Katika kundi lile, kila mmoja alikuwa anakula majani kwa “style” yake. Mbwa
Mwitu alikaa pembeni akiangalia wanavyokula majani
huku wakichezacheza
kurukaruka.
Alitamani sana Maisha yale.
Kilichomtamanisha ni
kuwa; Watoto wa Digidigi walikuwa mbele huku
mama zao wakiwa nyuma. Wanacheza na kula mbele
ya mama zao, ili ikitokea hatari waweze kunusurika.
Mbwa Mwitu alikatisha mawindo yake na kutamani
sana kujiunga nao, yaani kuwa kama wao. Hivyo,
aliomba nafasi ya kuonana na kiongozi wao.
Alipofika na kuongea naye alisema; nimekuwa
nikitamani kwa muda mrefu kuungana nanyi. Leo
naomba mnikaribishe rasmi niwe nanyi maana
nimependa “life style” yenu umoja na
mshikamano.
wa Digidigi akamuuliza Mbwa Mwitu;
mbona hufanani na sisi? Mbwa Mwitu akajibu;
nitajitahidi kuchonga na kuweka vipembe vidogo
vidogo kichwani na kupunguza mkia wangu na
masikio yangu. Pia nitajifunza kula nyasi ili niweze
kuendana nanyi. Kiongozi wa Mbwa Mwitu akasema;
sawa! Nenda ufanye hivyo, kisha urudi nione
utakavyokuwa unafanana.
Mbwa Mwitu akafanya kama alivyoambiwa, kisha
kurudi kwa kiongozi wa Digidigi. Alipofika alisema;
Mheshimiwa
tayari
nimeshajiweka
vizuri. Ona
nimepunguza mkia wangu, nimechongesha vipembe
na kupunguza upana wa masikio yangu. Lakini
kiongozi
alivyomtazama
akamwambia;
huwezi
kufanana na sisi. Miguu yako haina kwato kama yetu.
Mdomo wako upo tofauti na wa kwetu. Isitoshe,
ngozi yako ni tofauti na yetu. Sisi hatuna
mabakamabaka kama uliyonayo wewe. Sauti yako ni ya kubweka tofauti na ya kwetu. Tafadhali, tunaomba
uondoke hapa.
Mbwa Mwitu aliondoka akiwa amenyong’onyea
kurejea kwa Mbwa Mwitu wenzake. Alipofika
walimkataa,
kwa
sababu
tayari
alishabadili
mwonekano wake kuanzia kwenye masikio na mkia walimwambia ondoka kwetu. Wewe
sio mwenzetu umetusaliti. Mbwa Mwitu aliondoka
akiwa
na
machungu
mengi
na
kutokomea
kusikojulikana."
Tunachojifunza katika hadithi hii ni kuwa; katika safari yetu
ya kuelekea tunakohitaji, ambapo ndipo ndoto yetu ilipo,
tunapaswa kuthibiti baadhi ya tamaa zinazoweza kutupoteza
na kufanya tutoke kabisa katika mstari wetu wa utafutaji.
Tunapaswa kutoendekeza kuishi au kufanya kama wengine
wanavyofanya, bali tuweke nguvu katika vile tunavyoona ni
sahihi kutufikisha tunapokwenda.
Maelezo zaidi nimeweka katika kitabu Cha Ndoto Ya Maisha Yako.
Karibu sana tujifunze zaidi.
Mimi ni Lackius Robert
0767702659
#mwangaza2023.