Thursday, March 19, 2020

UCHAMBUZI WA KITABU CHA RICH DAD POOR DAD

Baada ya kumaliza utangulizi ,sehemu ya kwanza.

Karibu sasa katika sehemu ya pili Somo la kwanza:

SEHEMU YA PILI SOMO LA KWANZA: MATAJIRI HAWAFANYII KAZI PESA.

Siku moja nilimuuliza Baba tajiri je nawezaje kuwa tajiri?, Baba alishika karatasi na kalamu akainama uku akijikuna kichwa chake baadae akanijibu ,akisema mwanangu kwa nini unataka kuwa tajiri?. Nikasema mimi na Mike hatujashiriki sherehe ya rafiki yetu maeneo ya ufukweni sababu ya kutotuita ni kuwa sisi ni watoto maskini.Baba tajili akasema “ukitaka kuwa tajiri jifunze namna ya kutengeneza fedha’’.

Kipindi hicho nilikuwa nina miaka 9 ndipo urafiki na Mike ulianza tukaanza kufikiria namna ya kutengeneza fedha, lakini nakumbuka baba alisema ukihitaji  kitu fulani kifanyie kazi.Tulifanya kazi mbali mbali ikiwemo kuuza tooth paste tube lakini hatukufanikiwa kufika mbali ,ila kwa sababu baba tajiri alisema ukitaka kitu fulani lazima ufanye kazi ,niliutaka utajiri hivyo ilinibidi nijifunze jinsi ya kutengeneza fedha nikawa nafanya kazi masaa ya ziada matatu kwa baba tajiri na alikuwa ananilipa kiasi kidogo cha fedha.Wakati mwingine nilikuwa ninafanya na rafiki yangu Mike kazi zingine.Lakini sikuwahi kumwambiwa Baba masikini ambaye ni baba yangu mzazi kuwa nafanya kazi sehemu yoyote.

Nakumbuka Baba tajiri aliniambia  sababu kubwa kwanini matajiri ni matajiri sio kwa sababu ya tamaa bali wana woga  wa kupoteza fedha na kuwa maskini.Hivyo hutumia njia mbalimbali za kuhakikisha wanafahamu zaidi kuhusu fedha ili wazidi kuwa nazo zaidi na zaidi ukilinganisha na watu maskini.Pia anasema nimekuwa nakutana na watu katika sehemu tofauti wakisema ‘’sipendelei sana pesa ‘’ lakini watu hao hao wanafanya kazi masaa nane kwa siku ,je kama hawapendelei pesa kwanini  washinde wakifanya kazi masaa yote hayo?.Ukweli ni kuwa hisia ndizo zinazotufanya kuwa binadamu mfano mtu anaposema anatafuta kazi tayali hisia zake na fikra zinakuwa zinafikiria kazi akisema ninataka niwe tajiri hisia zake zitafikilia jinsi ya kuwa tajiri na akiaanza atafanikiwa.Mara nyingi wazazi wengi wamekuwa wakiandaa watoto wao katika mazingira ya kusoma kwa bidii kufaulu vizuri nakupata  kazi kwa hali hiyo tayali hisia zao zote zinawaza hivo.Jamii zetu ni kweli zinahitaji madaktari  wahasibu n.k lakini watu hawa wanapomaliza masomo yao wanafikiri shule imeishia hapo wanashindwa kujiedeleza kupata maarifa mengine hivyo wanakuwa hawana uelewa mzuri kifedha. Ndio maana wanaonekana kuwa na kazi nzuri kama Baba yangu maskini ana kazi nzuri lakini kutokana na kukosa maarifa ya fedha hujikuta ana mlundikano wa kodi nyingi.
Imeishia hapo.

Wewe ni wa thamani kubwa na kwa kuwa umeamua kujifunza ,tutajifunza pamoja.
Mungu akubariki.

Karibu sana tuwasiliane kupitia 0767702659 Lackius Robert kwa akili ya kupata uchambuzi wa vitabu vingine.

Monday, March 16, 2020

UCHAMBUZI WA KITABU CHA RICH DAD POOR DAD ROBERT KIYOSAKI



KITABU KINAITWA, RICH DAD AND POOR DAD, What the Rich teach their kids about money -that the Poor and  middle class do not!.( Baba tajiri baba maskini ,Jinsi matajiri wanavyofundisha watoto wao kuhusu Pesa ,kitu ambacho watu maskini na watu wa kipato cha kati hawafanyi.)

 MWANDISHI : ROBERT KIYOSAKI
MCHAMBUZI : LACKIUS ROBERT

Rich dad and Poor dad, Ni stori inayomhusu mwandishi Robert Kiyosaki aliyekuwa akiishi huko Hawaii akiwa na baba wawili yaani baba maskini (baba mzazi) na baba tajiri (asiye mzazi wake ).Baba maskini aliyekuwa mwajiriwa mwenye elimu ya juu na ajira kubwa pia baba tajiri aliyekuwa na elimu ndogo sana lakini ni mjasiriamali. Kiyosaki aliamua kufuata hatua za baba tajiri.

Lengo kuu la kitabu hiki ni kutoa ushauri na elimu ya uchumi ambayo Kiyosaki aliipata kutoka kwa baba tajiri.Anawafananisha na kuwatofautisha baba hawa kwa kuangalia ufanyaji wa kazi wao kwa bidii, kuelimika, kuwekeza, na namna ya kutafuta pesa.

UTANGULIZI:
Kuna huhitaji mkubwa wa watu kujua hili,
Mwandishi anaanza kwa kuuliza je shule zinawaandaa watoto kielimu kulingana na dunia ya leo?.
Wazazi wangu  waliniambia kuwa nenda shule soma sana pata alama nzuri upate kazi nzuri yenye manufaa.Malengo yao makubwa yalikuwa ni kutupa elimu nzuri ya chuo  mimi na dada yangu.Mwaka 1976 nilimaliza diploma na kuajiriwa kama mhasibu katika kiwanda kimoja.Mimi pamoja na Michael tulikuwa tukifanya kazi na kupandishwa vyeo mara kadhaa lakini kuongezeka kwa  mafao yetu yote kumekuwa kunategemea mchango wetu.Tumejaliwa kupata watoto watatu na wote tumewapa elimu nzuri.Siku moja mtoto wetu alikuja akiwa anaonekana kuboreka na shule akatuuliza hivi ‘’nimechoka kusoma masomo ambayo sitayafanyia kazi maishani mwangu’’. Bila kufikiria nikamjibu usipopata alama nzuri autaenda chuo, akaniuliza je nisipoenda chuo sitokuwa tajiri,nikamjibu usipoenda chuo autapata kazi na usipopata kazi autapata utajiri.
Watoto wengi siku hizi wanakuwa na kadi za benki hata kabla hawajaenda shule,pia wapo wafanyakazi wengi  wahasibu,wanasheria lakini bado hawana elimu ya msingi wa fedha na  hii ni kwa sababu shule zetu zinatufundisha kusoma kwa bidii,kupata alama nzuri,kwenda chuo na kupata kazi nzuri yenye mafao sio zaidi ya hapo.

Utangulizi unaishia hapo karibu uchangie.Kesho tunaenda sehemu ya kwanza.
 Baada kumaliza utangulizi hii ni sehemu ya kwanza.

Rich dad poor dad
 (BABA TAJIRI NA BABA MASIKINI),Katika sura hii anajaribu kuwaelezea vizuri baba wawili alionao ,naomba usome vizuri sehemu hii maana imebeba maana kubwa katika dhana nzima ya jinsi baba tajiri anavyofundisha watoto wake kuhusu fedha,na baba maskini anavyofundisha watoto wake kuhusu fedha.


Nina baba wawili mmoja masikini na mwingine tajiri.Mmoja amefanikiwa kusoma katika vyuo mbali mbali kama vile Stanfordbridge na vinginevyo pia ana elimu ya uzamili (PhD) mwingine hata darasa la nane hajamaliza.
Wote wamefanikiwa katika maeneo yao wapambanaji ,Wako vizuri wakalimu ,walinipa ushauri, lakini wa kitofauti mmoja anasema kupenda pesa ni chanzo cha maovu mwingine anasema ukosefu wa fedha ni chanzo cha maovu.Kuwa na wazazi wawili wenye ushauri huu wananitatiza kidogo.

Maana nawaza nichukue upi niache upi wamenifanya nikae nawaza kila wakati. Nimekuja kugundua kwamba sababu kubwa inayopelekea matajiri kuendelea kuwa matajiri ,wenye kipato cha kati kubakia pale pale na masikini kuendelea kuwa  maskini ni kwamba somo la elimu ya fedha linafundishwa nyumbani tu  sio shuleni.
Shuleni tunafundishwa kusoma na kufaulu zaidi baade kutafuta kazi mfano ukiwaangalia madaktari  ,wahasibu, wafanyakazi wa benki shuleni wamefauru vizuri lakini wanaagaika kupata pesa za kujikimu kwenye maisha yao.
Baba maskini  anasema soma sana utafute kampuni ukafanye kazi  ,Baba tajiri   anasema soma sana utafute kampuni ya kununua uwaajiri watu .Tena mwingine anasema sababu inayonifanya kuwa maskini ni kwa sababu niko na wewe mtoto ,mwingine anasema ninapaswa kuwa tajiri kwa sababu niko na wewe mtoto.

Naomba kuishia hapo unaweza kupata uchambuzi huu kutumia namba 0767702659
Lackius Robert karibu sana